07-Hadiyth Husnul-Khuluq: Husnul-Khuluq Ni Sababu Ya Kuingizwa Jannah

 

 

Hadiyth: Husnul-Khuluq (Tabia Njema)

 

Hadiyth Ya  7

 

Husnul-Khuluq Ni Sababu Ya Kuingizwa Jannah

 

Alhidaaya.com

 

 

 

عن أَبِي هُرَيْرَةَ‏:‏ سُئِلَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم‏:‏ مَا أَكْثَرُ مَا يُدْخِلُ الْجَنَّةَ‏؟‏ قَالَ‏:‏ ((تَقْوَى اللهِ، وَحُسْنُ الْخُلُقِ)) قَالَ‏:‏ وَمَا أَكْثَرُ مَا يُدْخِلُ النَّارَ‏؟‏ قَالَ‏:‏ ((الأَجْوَفَانِ‏:‏ الْفَمُ وَالْفَرْجُ‏.))

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa: “Jambo gani zaidi litakalokuwa ni sababu ya kumwingiza mtu Jannah?” Akasema: ((Taqwa (kumcha Allaah) na Husnul-Khuluq (tabia njema)). Na akulizwa: “Jambo gani zaidi litakalokuwa ni sababu ya kumwingiza mtu Motoni?” Akasema; ((Mdomo na sehemu za siri)) [Al-Adab Al-Mufrad, Swahiyh Ibn Maajah (3443)], Swahiyh At-At-Tirmidhiy (2004)]

 

Share