Hadithi Ya 20: Ikiwa Huna Haya Basi Fanya Utakavyo
الحديث العشرون
"إذا لم تستح فاصنع ما شئت"
عن أبي مَسْعُودٍ عُقْبَةَ بن عمرو الأَنْصَارِيّ البَدْرِيّ رضي اللهُ عنه قال : قالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((إِنَّ مما أَدْرَكَ النَّاسُ مِنْ كَلامِ النُّبُوَّةِ الأولَى: إِذا لمْ تَسْتَحِ فاصْنَعْ ما شِئْتَ)).
رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ
HADITHI YA 20
IKIWA HUNA HAYA
Kutoka kwa Abu Mas'ud ‘Uqbah Ibn 'Amr Al Ansariy Al Badriy رضي الله عنه ambaye amesema kuwa Mtume صلى الله عليه وسلم kasema: “Katika maneno ambayo watu waliyapata kutoka kwa Mitume wa mwanzo (waliotangulia) ni haya: “Ikiwa huna haya basi fanya utakalo.”
Imesimuliwa na Al-Bukhari
- Login or register to post comments
- Email this page


