063-Al-Munaafiquwn: Utangulizi Wa Suwrah

 

063-Al-Munaafiquwn: Utangulizi Wa Suwrah

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Imeteremka: Madiynah kwa itifaki ya ‘Ulamaa

 

Idadi Za Aayah: 11

 

Jina La Suwrah: Al-Munaafiquwn (Wanafiki)

 

Suwrah imeitwa Al-Munaafiquwn (Wanafiki), na inayodalilisha ni Hadiyth ifuatayo:

 

عن زَيدِ بنِ أَرْقَمَ رَضِيَ اللهُ عنه، قال ... فلمَّا أصبَحْنا قرأ رَسولُ اللهِ صلَّى اللهُ عليه وسلَّم سورةَ المُنافِقينَ

 

Amesimulia Zayd Bin Arqam (رضي الله عنه): “...... Tulipopambazukiwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasoma Suwrah Al-Munaafiquwn.” [At-Tirmidhiy na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh At-Tirmidhiy (3313)]

 

Na katika Hadiyth iliyotajwa katika Fadhila. Na pia kutajwa katika Aayah namba (1).

 

Miongoni Mwa Makusudio Ya Suwrah:

 

1-Kuubainisha uhakika wa wanafiki na kutahadharisha (Ummah) juu yao. [Al-Mukhtaswar Fiy Tafsiyr Al-Qur-aan Al-Kariym]

 

2-Makatazo ya kughafilika na Kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kushughulishwa na mali na watoto, na amrisho la kutoa mali katika Njia ya Allaah.  

 

Miongoni Mwa Maudhui Ya Suwrah:

 

1-Suwrah imefunguliwa kwa kuwaelezea wanafiki na kubainisha tabia zao mbaya, miongoni mwa uongo, na viapo vya uovu, uoga, na kuwazuia watu kutoa mali kuwasaidia Swahaba wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) waliohajiri.

 

2-Waumini waliamrishwa kutokuwaombea maghfirah wanafiki kwani Allaah Hakupenda kuwaghufuria.

 

3-Waumini wameamrishwa kutokushughulishwa na mali na watoto kutokana na Kumdhukuru Allaah na tahadharisho la kula khasara.

 

4-Suwrah imekhitimishwa kwa kuhimizwa Waumini kutoa mali kwa ajili ya Allaah na tahadharisho kuwa nafsi itakuja kutamani kurudi duniani ili mtu atoe mali yake aliyoiacha, lakini muda wa kufariki mtu haurudishwi nyuma!

 

Fadhila Za Suwrah:

 

Ni Sunnah Kuisoma Katika Rakaa Ya Pili Kwenye Swalaah Ya Ijumaa:

 

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ   أَنَّ اَلنَّبِيَّ ‏- صلى الله عليه وسلم ‏-كَانَ يَقْرَأُ فِي صَلَاةِ الْجُمُعَةِ سُورَةَ الْجُمُعَةِ وَالْمُنَافِقِينَ   رَوَاهُ مُسْلِم  

Amesimulia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما): Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akisoma katika Swalaah ya Ijumaa, Suwrah Al-Jumu’ah na Al-Munaafiquwn. [Muslim]

 

 

 

Share