072-Al-Jinn: Utangulizi Wa Suwrah

 

072-Al-Jinn: Utangulizi Wa Suwrah

 

Alhidaaya.com

 

 

Imeteremka: Makkah kwa itifaki ya ‘Ulamaa.

 

Idadi Za Aayah: 28

 

Jina La Suwrah: Al-Jinn

 

Suwrah imeitwa Al-Jinn (Majini), na inayodalilisha ni kutajwa kwake katika Aayah namba (1).

 

Miongoni Mwa Makusudio Ya Suwrah:

 

1-Kubatilisha dini ya washirikina, kwa kubainisha hali ya majini na imaan zao baada ya kuisikia Qur-aan. [Al-Mukhtaswar Fiy Tafsiyr Al-Qur-aan Al-Kariym]

 

2-Kutaja yanayofungamana na khabari za majini, na kusikiliza kwao Qur-aan, na mrejesho wao katika hilo, na kwa wale wenye kuitikia Amri za Allaah na wenye kuzipuuza.

 

Miongoni Mwa Maudhui Ya Suwrah:

 

1-Suwrah imefunguliwa kwa kutajwa majini  walivoisifia  Qur-aan kuwa ni ya ajabu, na inaongoza katika uongofu na wakaiamini.

 

2-Kisha wakamsifia Allaah (سبحانه وتعالى) kwa Ujalali Wake, na wakaahidi kutokumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) na wakampwekesha na kumtakasa kwamba Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee, Hahitaji kuwa na mke wala mwana! 

 

3-Ikaendelea kutajwa mazungumzo ya majini kukiri makosa na madhambi yao, na kuwatahadharisha majini wenzao kwa adhabu itakayowapata pindi wakipanda juu kusikiliza siri za mbinguni, na wakadhihirisha unyenyekevu wao.

 

4-Imetajwa vigawanyo vya majini kati ya wema na waovu, na kati ya Waislamu na makafiri.

 

5-Ikatajwa makatazo ya kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) na yeyote bali inapaswa Kumpwekesha katika ibaada zote zikiwemo za kuomba duaa.

 

6-Yametajwa mas-ala kadhaa kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ayabalighishe kwa watu na wakaonywa wale watakaomuasi Allaah (سبحانه وتعالى) na kuahidiwa makazi mabaya ya motoni wadumu humo.

 

7-Suwrah imekhitimishwa kwa kubainishwa Sifa Tukufu za Allaah za Ujuzi wa ghaibu na yaliyofichika na sifa hii hakuna yeyote mwenye kuimiliki isipokuwa Yeye Pekee (عزّ وجلّ). 

 

 

 

 

 

 

 

Share