097-Al-Qadr: Utangulizi Wa Suwrah

 

097-Al-Qadr: Utangulizi Wa Suwrah

 

Alhidaaya.com

 

 

Imeteremka: Makkah au Madiynah kwani ‘Ulamaa wamekhitilafiana kuhusu wapi imeteremshwa.

 

Idadi Za Aayah: 5

 

Jina La Suwrah: Al-Qadr

 

Suwrah imeitwa Al-Qadr (Qadar), na yanayodalilisha ni kutajwa kwake katika Fadhila, na pia kutajwa katika namba (1). Rejea kwenye Faida ya Aayah namba (1) ambako kuna maelezo kuhusu ‘Ulamaa kukhitilafiana maana ya Qadr.   

 

Miongoni Mwa Makusudio Ya Suwrah:

 

1-Kubainisha fadhila za Laylatul-Qadr. [Al-Mukhtaswar Fiy Tafsiyr Al-Qur-aan Al-Kariym]

 

2-Kutaja fadhila za usiku mtukufu kabisa, Laylatul-Qadr, na kuashiria kuteremshwa Qur-aan Usiku huo.

 

Miongoni Mwa Maudhui Ya Suwrah:

 

1-Suwrah imeanza kuelezewa kuteremshwa Qur-aan katika Layalatul-Qadr (Usiku wa Qadar), na kwamba usiku huo ni mtukufu mno, nao umo katika kumi la mwisho la mwezi wa Ramadhwaan.  

 

2-Ikaendelea kuelezwa na kukhitimishwa kwa kubainishwa kwamba usiku huo ni mbora kuliko miezi elfu moja, na kwamba Malaika wengi pamoja na Jibriyl (عليهم السّلام) wanateremka kwa Idhini ya Rabb wao kwa kila jambo Alilolikadaria mwaka huo, na kwamba usiku wote huo hakuna shari, bali kuna amani mpaka kutokea Alfajiri.  

 

 

Share