02-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kuridhika na kuwa na subira kwa Qadar ya Allah (Subhaanahu wa Ta'ala)

Kuridhika na kuwa na subira kwa Qadar ya Allah (Subhaanahu wa Ta'ala)
 
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, ‘ Ajabu kwa mambo ya muumini, kila kitu kwake ni la kheri, na hiyo ni kwa muumini peke yake tu, yakimfika yenye kufurahisha hushukuru na hiyo huwa ni kheri kwake, na yakimsibu madhara husubiri na hivyo kuwa ni kheri kwake’ (Muslim)
 
Waliokuwa pambizoni mwake ni juu yao kumkumbusha hilo mara kwa mara na wamhimize nalo bali waoneshe mfano kwake katika kusubiri na kuridhisha.
Share