25-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Maombolezo yaliyoharimishwa

 

Maombolezo yaliyoharimishwa:

 

Huku ni kuomboleza kijaahiliya, kama vile kutaja amali za aliyefariki kama kutaja mazuri yake, ushujaa wake na mengine aliyoyafanya, kama vile tuonavyo leo hii katika magazeti na majarida au katika matangazo mbali mbali. Haya ndiyo maombolezo ya Kijaahiliya ambayo Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) ametukataza, na jambo hili linaingia katika jumla ya maombolezo na kelele ambazo zinamdhuru maiti na watu wake wala hayawanufaishi na chochote.

Share