34-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Dua zilizopokelewa katika dua za Jeneza

Du'aa zilizopokelewa katika dua za Jeneza:
 
 
Kutoka kwa 'Awf bin Maalik (Radhiya Allaahu 'anhu) amesema, ‘Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) aliliswalia Jeneza nikahifadhi du'aa yake alipokuwa akiomba,
 
 
اللهُـمِّ اغْفِـرْ لَهُ وَارْحَمْـه، وَعافِهِ وَاعْفُ عَنْـه، وَأَكْـرِمْ نُزُلَـه، وَوَسِّـعْ مُدْخَـلَه، وَاغْسِلْـهُ بِالْمـاءِ وَالثَّـلْجِ وَالْبَـرَدْ،
وَنَقِّـهِ مِنَ الْخطـايا كَما يُنَقََّ الـثَّوْبُ الأَبْيَـضُ مِنَ الدَّنَـسْ، وَأَبْـدِلْهُ داراً خَـيْراً مِنْ دارِه، وَأَهْلاً خَـيْراً مِنْ أَهْلِـه،
وَزَوْجَـاً خَـيْراً مِنْ زَوْجِه،  وَأَدْخِـلْهُ الْجَـنَّة، وَأَعِـذْهُ مِنْ عَذابِ القَـبْر وَعَذابِ النّـار
 
“Allahumma ighfir lahu warhamhu, Waafihi waafu anhu, wa’akrim nuzulahu, wawasigh madkhalahu, wa’aghsiluhu bil maai wathalji walbarad, wanaqihi minal khatwaaya kama Yunaqa thawbul abyadhu mina ddanas, wa abdil-hu daaran khayran min daarihi, wa ahlan khayran min ahlihi, wazawjan khayran min zawjihi, wa adkhil-hul Jannah, wa a'idh-hu min ’adhabil Qabri, wamin 'adhaabin nnaar.”Anaendelea kusema Maalik, ‘Nikatamani kuwa mimi ndio niwe yule maiti anayeswaliwa.”  
 
Kutoka kwa Zaid bin Rukaana bin Abdul Mutwalib amesema, ‘Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) anaposimama kuliswalia jeneza husema, “Allahumma abduka wa ibn Amatak ahtaaj ila rahmatika, wa anta ghaniyu ‘an 'adhaabihi, Inn kaana muhsinan fazid fi hasanaatih, wain kaana musiian fatajaawaz ‘anhu.” (Al-Haakim)
Wakati fulani aliulizwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu), ‘Ni vipi kuswalia Jeneza? Abu Hurayrah Allahumma inahu 'abdika wa ibn 'abdika wa ibn amatika, kaana yashhadu an laa ilaaha illa Allaahu, wa ana Muhammadan 'abduka wa rasuuluka, wa anta a’lamu bihi, Allahumma in kaana muhsinan fazid fii hasanaatih wa in kaana musiian fatajaawaz 'an sayiatihi, Allahumaa laa tuharimna ajrahu wala tuftina ba'dahu.” (Maalik)
 
Share