26-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Wajibu Wa Waliymah (Karamu)

Mume lazima afanye karamu baada ya kufunga ndoa.  Hii ni kutokana na amri ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliyompa 'Abdur-Rahmaan ibn 'Awf afanye na pia kutokana na Hadiyth iliyosimuliwa na Buraydah ibn Hasiyb ambaye amesema:

 

لَمَّا خَطَبَ عَلِي فَاطِمَةُ رَضِيَ الله عَنْهُ قال: قال رَسُولُ الله صَلَّى الله عَلَيْهِ وَسَلَّمْ:  (( إِنَّهُ لاَ بُدَّ لِلْعرْس  مِنْ وَلِيمَة )) وَفِي رِوَايَة ((لِلْعَرُوس))

"'Aliy alipomposa Faatwimah alisema: Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema: ((Hapana budi iwepo karamu, hapana budi bwana harusi afanye karamu)). Msimuliaji amesema: Sa’ad akasema, mimi nitaleta kondoo, na mwingine akajitokeza akasema, mimi nitaleta kadha wa kadha katika mahindi. Katika Riwaaya nyingine ma-Answaar walikusanya mahindi mengi[1]

 

 


[1] Ahmad na At-Twabaraaniy: Isnaad yake inakubalika kama alivyosema Al-Haafidhw Ibn Hajar katika Fathul-Baariy 9/188

Share