03-Uswuul Al-Fiqhi: Utangulizi

Sayansi ya Usuul al-Fiqh, hakika inaeleweka kuwa ni njia muhimu sana ya uchunguzi ambayo imepata kuvumbuliwa na mawazo ya Waislamu. Hakika, kwa vile ni msingi madhubuti ambao juu yake nidhamu za Kiislamu zimeegemezwa, Uswuul al-Fiqh sio tu imenufaisha ustaarabu wa Kiislamu, lakini umechangia kuwa ni maandiko mazuri kabisa kwa ustaarabu wa dunia kwa jumla. Haitokuwa sehemu ya nje kueleza hapa namna utaratibu wa kufananisha ulivyoendelezwa ndani ya kuta za Fiqhi ya Kiislamu.

 

Tunaiwasilisha kazi hii fupi, kwa wote walio na hamu ya kuongeza elimu fulani kwenye sayansi hii. Na tunamuomba Allaah Ta’ala Atusaidie sisi na kutunufaisha kwa tuliyoelimika na kuelimika kwa yale tuliyonufaika, na kutulinda sisi kutokana na elimu isiyo na manufaa, na kutokana na vitendo ambavyo havikubaliki Kwake. Wa Akhiru Da’wana an al Hamdu Lillah Rabb al ‘Alamiyn (Sifa zote na shukrani zote ni zake Allaah, Bwana na mlinzi wa viumbe vyote).

 

 

 

Share