02-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Zakaatul-Fitwr Apewe Nani?

 Zakaatu-Fitwr Apewe Nani?

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI

 

Zakaatul-Fitwr apewe nani? Je, inaruhusiwa kuituma mfano kwa Mujaahidiyn waliko vitani? Au kuitoa katika vyama vinavyokusanya sadaka au kujengea msikiti?

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah

 

Zakaatul-Fitwr inapaswa kupewa maskini Waislamu katika nchi au mji ambao inatolewa kwa sababu ya usimulizi wa Abuu Daawuwd kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ambaye amesema: "Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameamrisha Zakaatul-Fitwr ilipwe Ramadhwaan kuwalisha watu masikini…."

 

Inaruhusiwa kuituma kwa masikini wa nchi nyingine ambao watu wake wanahitaji zaidi. Hairuhusiwi kujengea msikiti au kuitoa katika miradi ya sadaka.

 

 

[Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah]

 

 

 

Share