24-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Wakati Gani Zakaatul-Fitwr Itolewe? Na Muda Gani Mwisho Kutoa?

 

 Wakati Gani Zakaatul-Fitwr Itolewe? Na Muda Gani Mwisho Kutoa?

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Je, wakati za kutoa Zakaatul-Fitwr ni kuanzia Swalah hadi siku inapomalizika? (Siku ya 'Iyd?)

 

JIBU:

 

 

Wakati wa kutoa Zakaatul-Fitwr sio inapoanza Swalaah ya 'Iyd bali inaanza kutoka jua linapozama siku ya mwisho ya Ramadhwaan ambayo ni usiku wa mwanzo wa mwezi wa Shawwaal na unamalizikia na Swalaah ya 'Iyd. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameamrisha kwamba itolewe kabla ya Swalaah. Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhuma) amesimulia kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakeyeitoa kabla ya Swalaah itakuwa ni Zakaah iliyokubaliwa (Zakaatul-Fitwr) na atakayeitoa baada ya Swalaah itakuwa ni sadaka ya kawaida)) [Abu Daawuwd 2/262-263, Namba 1609, Ibn Maajah 1/585, namba 1827, Ad-Daaraqutwniy 2/138, Al-Haakim 1/409]

 

Inaruhusiwa kuitoa siku moja au mbili kabla kutokana na dalili kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allahu anhumaa) ambaye amesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliamrisha Swadaqah ya Fitwr katika Ramadhaan)) na katika usimulizi mwengine walikuwa wakilipa siku moja au siku mbili kabla ya kumalizika Ramadhwaan.

 

Atakayechelewa kuitoa ukapita muda wake atakuwa amepata dhambi na itabidi afanye tawbah kwa kuchelewesha kuwapa masikini.

 

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

[Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah (2896)]

 

 

 

Share