Haki Za Mume Na Mke
Ummu Iyyaad
Mwanamume na mwanamke wanapofunga ndoa inawapasa wote watambue desturi, mwendo mwema na adabu katika maisha hayo ya mke na mume ili ndoa
Allaah سبحانه وتعالى anasema:
((وَلَهُنَّ مِثْلُ الَّذِي عَلَيْهِنَّ بِالْمَعْرُوفِ وَلِلرِّجَالِ عَلَيْهِنَّ دَرَجَةٌ وَاللّهُ عَزِيزٌ حَكُيمٌ))
{Nao wanawake wanayo haki kwa Sharia
Aya hii tukufu inatufundisha wazi kuwa mume na mke wote wana haki baina
قال رسول الله صلى الله عليه وسلم عند ما وقف في عرفة في حجة والوداع :(( يآ أيها الناس إن لنسائكم عليكم حقاً ولكم عليهن حق)) أبو داود
Mtume صلى الله عليه وسلم alisema aliposimama Arafa katika hutuba yake ya mwisho ya Hajj ((Ee nyie watu, hakika nyinyi mna haki juu ya wake zenu na wake zenu wana haki juu yenu)) (Abu Dawud )
Baadhi ya haki hizo ziko sawa baina ya mume na mke na nyinginezo ziko tofauti baina
HAKI ZA MUME NA MKE BAINA
Zifuatazo ni haki ambazo zinawapasa wote wawili wazitimize baina
1. Ukweli:
Jambo hili linawabidi wote wawili walitimize baina yao, ili upatikane utulivu wa kuaminiana baina
2. Mapenzi na huruma baina
Mapenzi katika ndoa ni jambo muhimu kuweko kwani bila ya kuweko bila shaka ndoa itakuwa yenye upungufu na ikawa sio imara bali huenda ikavunjika kutokana na sababu ya upungufu huu wa mapenzi baina ya mume na mke. Kila mmoja awe na mapenzi ya dhati kwa mwenzake hata ipatikane raha ya nafsi na maridhio baina
Allaah سبحانه وتعالى Amesema
((وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِّتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُم مَّوَدَّةً وَرَحْمَة ًإِنَّ فِي ذَلِكَ لَآ يَاتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ))
{Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao fikiri}. (Ar-Ruum 30:21)
3. Uaminifu:
Kila mmoja wao awe muaminifu kwa mwenzake hata isiwekodhana mbaya au shaka baina
Kila mmoja atambue kuwa yeye ni kioo na nafsi ya mwenzake, kwa hivyo vipi mtu asiweze kuwa muaminifu wa nafsi yake?
4. Tabia njema
Wawe na tabia njema na upole katika kauli na matendo ili iwepo heshima baina yao kama Alivyosema Allaah
(( وَعَاشِرُوهُنَّ بِالْمَعْرُوفِ))
{Na kaeni nao kwa wema} An-Nisaa 4:19
Kauli hii ya Allaah سبحانه وتعالى imekamilishwa na kauli ya Mtume صلى الله عليه وسلم
(Nakuusieni kuwafanyia wema wanawake ) Al Bukhari na Muslim
5. Kuhifadhiana siri na aibu
Haiwapasi wote kutoleana siri zao au kutoa aibu zao kwa watu wengine bali kila mmoja ahifadhi heshima ya mwenziwe kwa watu wa nje.
Mtume صلى الله عليه وسلم kasema {Watu watakaokuwa katika hali mbaya kabisa mbele ya Allaah سبحانه وتعالى siku ya Kiyama ni mwanamme anaekwenda kwa mke wake na mke kwa mume wake kisha akapita kutoa siri yake } Muslim
Hizo kwa ujumla ni desturi na haki ambazo zinapaswa kutekelezwa sawa sawa baina ya mume na mke kwani walikwishachukua ahadi nzito ya Allaah :
((وَكَيْفَ تَأْخُذُونَهُ وَقَدْ أَفْضَى بَعْضُكُمْ إِلَى بَعْضٍ وَأَخَذْنَ مِنكُم مِّيثَاقًا غَلِيظًا))
{Na mtachukuaje na ilhali mmekwisha ingiliana nyinyi kwa nyinyi, na wao wanawake wamechukua kwenu ahadi iliyo madhubuti?} An-Nisaa:20
Vile vile hivi itakuwa wametimiza kumtii Allaah سبحانه وتعالى katika kauli yake :
((وَلاَ تَنسَوُاْ الْفَضْلَ بَيْنَكُمْ إِنَّ اللّهَ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ))
{Wala msisahau fadhila baina yenu. Hakika Mwenyezi Mungu anayaona mnayo yatenda}. Baqarah 2:237
Zifuatazo ni haki ambazo zinampasa mmojawao azitimize kwa Mwenzake:
HAKI ZA MKE KUTOKA KWA MUME
1. Ni wajibu wa mume kumlisha mkewe anapokula yeye, kumvisha anapovaa yeye na kumtimizia mahitajo yake ya nyumbani.
2. Mume vile vile ni wajibu wake kumtia adabu mke anapohisi uasi wa mke wake
وَاللاَّتِي تَخَافُونَ نُشُوزَهُنَّ فَعِظُوهُنَّ وَاهْجُرُوهُنَّ فِي الْمَضَاجِعِ وَاضْرِبُوهُنَّ فَإِنْ أَطَعْنَكُمْ فَلاَ تَبْغُواْ عَلَيْهِنَّ سَبِيلاً إِنَّ اللّهَ كَانَ عَلِيًّا كَبِيرًا
{Na ambao mnachelea kutoka katika ut'iifu wanasihini, muwahame katika malazi na wapigeni. Wakikut'iini msiwatafutie njia ya kuwaudhi bure. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye aliye juu na Mkuu} (An-Nisaa
Aya hii inataka maelezo kidogo kwani baadhi wa wanaume wameifahamu sivyo Allaah سبحانه وتعالى Aliposema "muhame katika malazi na wapigeni"
Ibn Abbas na wengineo wamesema kuwa Aya imemaanisha kupiga mpigo usio mkali (yaani mpigo hafifu) Al-Hassan Al- Basri kasema kuwa ina maana mpigo usio wa nguvu.
Maulamaa wameelezea maana hasa ya kauli hii kwamba inamaanisha :
a)
b) Atakapoendelea kutokumtii mume wake basi awe mbali nae kitandani, yaani asiwe analala nae kwa muda hivi wala asiseme nae mpakamke ahisi vibaya ajue kuwa kweli mumewe kakasirika nae, Pindi mke akikubali makosa yake basi yawe vile vile yamekwisha warudie hali yao kama kawaida .
c) Kisha tena ikiwa bado mke hana utiifu, hapa sasa mume anaweza kumpiga mkewe. Lakini sio kumpiga kwa nguvu
في صحيح مسلم عن جابر عن النبي صلى الله عليه وسلم : أنه قال في حجة الوداع :
واتقوا الله في النساء فإنهن عندكم عوان ولكم عليهن ألا يوطئنفرشكم أحدا تكرهونه
فإن فعلن ذلك فاضربوهن ضربا غير مبرح ولهن عليكم رزقهن وكسوتهن بالمعروف
Imepokelewa na Muslim kutoka kwa Jabir kwamba Mtume صلى الله عليه وسلم kasema katika Hijja ya kuaga {Mcheni Allaah kwa wanawake kwani wao ni wasaidizi wenu. Mnayo haki juu
3. Ni wajib wake mume kumpa mafundisho ya dini mke wake anayoyahitaji
((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا))
((Enyi mlio amini! Jilindeni nafsi zenu na ahali zenu na Moto)) (At Tahriim 66:6)
4. Ni wajibu wake mume kumrekebisha mkewe anapokosea kufuata sharia za dini yake kama kuhakikisha mavazi ya stara na kuitimiza hijaab, vile vile asimwachie kuchanganyika na wanaume isipokuwa wale waliokuwa kaharimishwa nao.
5. Ni wajibu wake kumhifadhi kwa kila njia. Mume awe ndio mlinzi wake na mwenye majukumu kwake katika mambo yake yote
(( الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاء))
{Wanaume ni wasimamizi wa wanawake} An-Nisaa 34
{ Mtume صلى الله عليه وسلم kasema : Mwanamme ni mchunga (msimamizi) wa nyumbani kwake na ataulizwa kuhusu uchungaji (usimamizi) wake} Al-Bukhari na Muslim
6. Ikiwa mume ana mke zaidi ya mmoja, inampasa afanye uadilifu baina ya hao wake katika matumizi yao ya chakula, nguo, maskani na kadhalika. Allaah سبحانه وتعالى kakataza kutokuadilisha kwa kusema
((فَإِنْ خِف ْتُمْ أَلاَّ تَعْدِلُواْ فَوَاحِدَةً أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ذَلِكَ أَدْنَى أَلاَّ تَعُولُواْ))
{na mkiogopa kuwa hamwezi kufanya uadilifu, basi (oeni) mmoja tu, au wale ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki. Kufanya hivi ndiko kutapelekea kutokufanya jeuri} An-Nisaa 4:3
Juu ya hivyo Mtume صلى الله عليه وسلم aliusia kuwa wanawake watendewe mema
{Mbora wenu ni yule Aliye mbora kwa familia yake na mimi ni mbora kabisa kwa familia yangu} At-Tabarani
HAKI ZA MUME KUTOKA KWA MKE
1. Mke ajue umuhimu wa kumtii mume wake kuwa ni jambo muhimu na kutokumtii ni jambo la hatari kwani hadithi inasema :
((لَوْ كُنْتُ آمِراً أَحَداً أَنْ يَسْجُدَ لأَِحَدٍ لأَمَرْتُ الْمَرْأَةَ أَنْ تَسْجُدَ لِزَوْجِهَا مِنْ عِظَمِ حَقَِّهِ عَلَيْهاَ))
{Mtume صلى الله عليه وسلم kasema "
2. Mke inampasa kumtimizia haja ya mumewe wakati wowote anapomhitajia kujimai naye, kwani kuna hatari kwa kutokumtii mumewe katika jambo hili
((إذا دَعَا الرَّجُلُ امْرَأتَهُ إِلىَ فِرَاشِهِ فَأَبَتْ عَلَيْه لَعَنَتْهَا الْمَلائِكَةُ حَتَّى تُصْبِحَ))
{Mume atakapomwita mkewe kitandani na akikataa mke, basi malaika watakuwa wanamlaani huyo mke mpaka asubuhi} Imepokelewa na Imam Al-Bukhari
3. Kumhudumia mumewe kwa upole (yaani bila ya kujikalifisha zaidi ya uwezo wake)
4. Haimpasi mke kutoa sadaka kitu chochote bila idhini ya mumewe . Kasema Mtume صلى الله عليه وسلم
} قال صلي الله عليه وسلم " لا تنفق المرأة من بيتها شيئا إلا بإذن زوجها قالوا يا رسول الله ولا الطعام قال ذلك من أفضل أموالنا{
صحيح ابن ماجه - (حديث حسن الألباني)
{Asitoe sadaka mwanamke kitu chochote kutoka nyumbani ila kwa idhini ya mumewe. Wakasema ewe Mjumbe wa Allaah hata chakula? Kasema hicho ni
Ama mwanamke anayo haki kutoa sadaka katika kipato chake mwenyewe kisicho cha mumewe.
Katika hadithi nyingine sahihi inatujulisha kuwa mwanamke anaweza kutoa sadaka ikiwa anatambua kuwa hatoghadhibikiwa na mumewe.
((عن همام قال سمعت أبا هريرة رضي اللهم عنهم عن النبي صلى اللهم عليه وسلم قال إذا أنفقت المرأة من كسب زوجها عن غير أمره فله نصف أجره)) - البخاري
Kutoka kwa Hamaam kasema : {Nimemsikia Abu Hurayra رضي اللهم عنهم kwamba Mtume صلى الله عليه وسلم kasema {mwanamke akitoa sadaka kutoka katika kipato cha mumewe bila ya amri yake basi na yeye atapata thawabu nusu yake } Al-Bukhari
5. Haimpasi mwanamke kutoka nyumbani kwake bila ya idhini ya mumewe. (hata kwenda kwa wazazi wake)
6. Haimpasi mwanamke kumfanyia ujeuri, ufedhuli au usafihi mumewe
(عن عبد الرحمن ابن عوف قال قال رسول الله صلى اللهم عليه وسلم إذا صلت المرأة خمسها وصامت شهرها وحفظت فرجها وأطاعت زوجها قيل لها ادخلي الجنة من أي أبواب الجنة شئت) صحيح الترغيب
{Kutoka kwa Abdur-Rahman Ibn 'Awf kasema: Kasema Mtume صلى الله عليه وسلم : Atakaposwali mwanamke Swalah zake tano, akafunga mwezi wake (wa Ramadhaan), akahifadhi sehemu zake za siri (asifanye uzinifu), akamtii mume wake, ataambiwa ingia peponi kupitia mlango wowote autakao ) Sahih Targhiib
Bila ya shaka baada ya kutimiza haki hizi, ndoa itakuwa yenye kudumu bila ya kuwa na matatizo makubwa ya kuiharibu au kuivunja نَعُوذُ بالله (Tunajikinga kwa Allaah)
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


