Taratibu Za Ruqyah Na Yapasayo Kufanywa Kabla Ya Kusoma Ruqyah
SWALI:
Nimepitia website yenu nzuri mashAllaah, Mungu awazidishie na kazi hiyo nzuri. Tafadhali kuhusu suala la Rukyah, tafadhali nitumie utaratibu kamili, yaani ayas na sura za rukyah zote na utaribu wa kuzisoma hizo sura. Pia nielimishe vipi nitajiyarisha ninapo jisomea rukyah, yaani kuhusu udhu, mavazi na kadhalika. Shukran
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako
Ama njia ya kujikinga mwenyewe ni kuwa uwe unasoma Aayah zifuatazo asubuhi na jioni. Nazo ni
- Al-Faatihah (Surah ya kwanza).
- Al-Baqarah (Aayah nne za mwanzo, Ayatul Kursiy na Aayah mbili baada yake na Aayah tatu za mwisho).
- Aal-‘Imraan (3: 1 – 2).
- Suratut Tawbah (9: 129 mara saba).
- Al-Israa’ (17: 110 – 111).
- Al-Mu’minuun (23: 115 – 118).
- Al-Hashr (59: 22 – 24).
- Al-Kaafiruun (109).
- Al-Ikhlaasw, al-Falaq na an-Naas (mara tatu tatu).
Ama kipengele cha pili cha kumsomea mwengine inafaa usome Aayah zifuatazo:
Mwanzo unaanza na A’udhu Billaahi minash Shaytwaanir Rajiym.
- Al-Faatihah (Surah ya kwanza).
- Al-Baqarah (ayah 1 – 5, 102, 163 – 164, 255, 285 - 286).
- Aal-‘Imraan (3: 18 – 19).
- Suratut al-A‘raf (7: 54 – 56, 117 - 122).
- Yunus (10: 81 – 82).
- Twaaha (20: 69).
- Al-Hajj (22: 19 – 22).
- Al-Mu’minuun (23: 115 – 118).
- An-Naml (27: 30 – 31).
- Asw-Swaaffaat (37: 1 – 10).
- Ad-Dukhkhaan (44: 43 – 48).
- Al-Ahqaaf (46: 29 – 32).
- Al-Fath (48: 29).
- Ar-Rahmaan (55: 33 – 36).
- Al-Hashr (59: 21- 24).
- Al-Jinn (72: 1 – 9,
- Al-Buruuj (85).
- Zilzalah (99).
- Al-Humazah (104).
- Al-Ikhlaasw, al-Falaq na an-Naas.
Ama unapokuwa unasoma unafaa uwe twahara (nguo na mwili) na umejisitiri kwa kujifunika vizuri sehemu zipasazo kusitiriwa na pia usome kwa unyenyekvu.
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


