Hadiyth Ya 21 - Nimeikataza Nafsi Yangu Dhulma Na Nimeiharamisha Kwenu
Hadiyth Ya 21
Nimeikataza Nafsi Yangu Dhulma Na Nimeiharamisha Kwenu
Kwa Hivyo Msidhulumiane
عن أبي ذَرٍّ الْغِفاريِّ رضي الله عنه، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم فيما يَرْويهِ عن رَبِّهِ عَزَّ وجَلَّ أَنَّهُ قال:
(( يا عِبادي إنِّي حَرَّمْتُ الظُلْمَ على نَفْسِي وَ جعَلْتُهُ بَيْنَكُمْ مُحَرَّماً فلا تَظَالَمُوا.
يا عِبادي كُلُّكُمْ ضالٌّ إلا مَنْ هَدَيْتُهُ، فاسْتَهدُوني أهْدِكُمْ.
يا عِبادِي كُلُّكُمْ جائعٌ إلا مَنْ أطْعَمْتُهُ، فاسْتَطْعِمُوني أُطْعِمْكُم.
يا عِبادِي كُلُّكُمْ عَارٍ إلا مَنْ كَسَوْتُهُ، فاسْتكْسوني أَكسُكُم.
يا عِبادِي إِنَّكُمْ تُخْطِئُونَ بالليْلِ والنَّهارِ، وأنا أَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَميعاً، فاسْتَغْفِرُوني أُغْفِر لكُمْ.
يا عِبادِي إِنَّكُمْ لنْ تبْلغُوا ضُرِّي فتَضُرُّوني، ولن تبْلُغُوا نفْعي فَتَنْفعُوني.
يا عِبادِي لوْ أَنَّ أَوَّلَكُمْ وآخِرَكُمْ وإنْسَكُمْ وجِنَّكُمْ كانُوا عَلَى أَتْقَى قَلْبِ رَجُلٍ واحدٍ مِنْكُمْ ما زادَ ذلك في مُلْكي شَيئاً.
يا عِبادِي لوْ أَنَّ أَوَّلكُمْ وآخِرَكُمْ وإنْسَكُمْ وجِنَّكُمْ كانُوا عَلَى أَفْجَرِ قَلْبِ رَجُلٍ وَاحدٍ مِنْكُمْ ما نَقَصَ ذَلِكَ مِنْ مُلْكي شَيئاً.
يا عِبادِي لوْ أَنَّ أَوَّلَكُمْ وآخِرَكُمْ وإنْسَكُمْ وجنَّكُمْ قاموا في صَعِيدٍ وَاحِدٍ، فَسَأَلُوني، فأَعْطَيْتُ كلَّ واحدٍ مَسْأَلَتَهُ ما نَقَصَ ذلك مِمَّا عِنْدِي إلا كما يَنْقُصُ الْمِخْيَطُ إذا أُدْخِلَ الْبَحْرَ.
يا عِبادِي إنَّما هي أعمَالُكُمْ أُحْصِيها لَكُمْ ثُمَّ أُوَفِّيكُمْ إيَّاها، فَمَنْ وَجَدَ خيْراً فَلْيَحْمَدِ اللهَ، ومَنْ وَجَدَ غَيْرَ ذلك فَلا يَلومَنَّ إلا نَفْسَه)) رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abu Dharr Al-Ghifaariy رضي الله عنه naye kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وسلم akisimulia yale aliyopokea kutoka kwa Mola wake عَزَّ وَجَلَّkwamba: ((Enyi waja Wangu, Nimeikataza nafsi Yangu dhulma na Nimeiharamisha kwenu (hiyo dhulma), kwa hivyo msidhulumiane.
Enyi waja Wangu, nyote mumepotea isipokuwa wale Niliowaongoza, kwa hivyo tafuteni muongozo kutoka Kwangu Nitakuongozeni.
Enyi waja Wangu nyote mna njaa isipokuwa wale Niliowalisha, kwa hivyo tafuteni chakula kutoka Kwangu na Nitakulisheni.
Enyi waja Wangu, nyote mko uchi isipokuwa wale niliowavika nguo, kwa hivyo tafuteni vazi kutoka Kwangu Nitakuvisheni.
Enyi waja Wangu, mnafanya makosa usiku na mchana, na Ninasamehe dhambi zote, kwa hivyo tafuteni msamaha kutoka Kwangu Nitakusameheni.
Enyi waja Wangu hamuwezi kunidhuru Mimi wala kuninufaisha.
Enyi waja Wangu, ingekuwa wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu, binaAadamu katika nyinyi na majini katika nyinyi akawa mcha Mungu
Enyi waja Wangu, angelikuwa wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu, binaAadamu katika nyinyi na majini katika nyinyi akawa mbaya
Enyi waja Wangu ingelikuwa wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu, binaAadamu katika nyinyi na majini katika nyinyi mkasimama pahala pamoja na mkaniomba, na Nikawapa kila mmoja alichoomba, haitonipunguzia katika nilicho Nacho zaidi kuliko sindano inavyopunguza bahari inapochovywa.
Enyi waja Wangu, ni vitendo vyenu ninavyovihesabu, kwa ajili yenu Nikakulipeni. Kwa hivyo anayekuta wema amshukuru Allaah na yule anayekuta yasiyokuwa mema (basi) ajilaumu mwenyewe)) [Muslim]
- Login or register to post comments
- Email this page


