Hadiyth Ya 34 - Mwenye Kufurahi Na Kuchukia Kukutana Na Allaah
Hadiyth Ya 34
Mwenye Kufurahi Na Kuchukia Kukutana Na Allaah
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((قَالَ اللَّهُ إِذَا أَحَبَّ عَبْدِي لِقَائِي أَحْبَبْتُ لِقَاءَهُ وَإِذَا كَرِهَ لِقَائِي كَرِهْتُ لِقَاءَهُ))
البخاري و مالك
Kutoka kwa Abu Hurayrahرضي الله عنه ambaye amesema kwamba Mtume صلى الله عليه وسلم amesema: ((Allaah سبحانه وتعالى Amesema: Mja wangu akipenda kukutana na Mimi, Nami hupenda kukutana naye; na akiwa hapendi kukutana na Mimi, basi nami sipendi kukutana naye)) [Al-Bukhaariy na Maalik]
- Login or register to post comments
- Email this page


