Kauli Ya Swahaba Juu Ya Baadhi Ya Aya Katika Qur'aan
21 Rajab 1426
Aya tulizozitaja kuhusu nafsi itakavyojuta kwa kusema 'Ya hasrataa" (Ee majuto yangu) ambazo ziko katika Suratuz-Zumar zimetangulizwa na aya ambao ni aya ya pekee katika Qur'aan nzima yenye kutia matumaini baada ya mwanaadam kukosea nayo ni:
}}قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَى أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّهِ إِنَّ اللَّهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ{{
{{Sema: Enyi waja wangu walio jidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu}} Az-Zumar: 53
Imetoka kwa Shutayr bin Shakal ambaye kasema kwamba; Nimemsikia Ibn Ma'suud رضي الله عنه akisema;
Aya tukufu kabisa katika kitabu cha Allaah سبحانه وتعالى ni
}}اللّهُ لاَ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّوم{{
{{Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye Aliye hai, Msimamia mambo yote milele}} Al-Baqarah: : 255
Aya iliyokuwa na ufafanuzi kabisa kuhusu mazuri na maovu ni;
}}إِنَّ اللّهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالإِحْسَانِ{{
{{Hakika Mwenyezi Mungu anaamrisha kufanya uadilifu, na hisani}} An-Nahl:90
Aya yenye kuonyesha matumaini makubwa kabisa ni:
}}قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَى أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّه{{
{{Sema: Enyi waja wangu walio jidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu}} Az-zumar:53
Aya iliyokuwa ni dhahiri kabisa katika kumtegemea Allaah سبحانه وتعالى ni:
}}وَمَن يَتَّقِ اللَّهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا{{
}}وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ{{
{{Na anaye mcha Mwenyezi Mungu humtengezea njia ya kutokea}}
{{Na humruzuku kwa jiha asiyo tazamia}} At-Talaaq: 2-3
Masruuq akamwambia (Shutayr bin Shakal); Umesema kweli (kwamba kauli hiyo kasema Ibn Mas'uud رضي الله عنه )
(At-Tabaraniy 9:142)
*********
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


