Pilau ya Nyama ya Kusaga Na Mboga Mchanganyiko

 Pilau ya Nyama ya Kusaga na Mboga Mchanganyiko

 

Vipimo

Mchele - 2 Mugs       

Viazi - 3

Nyama ya Kusaga - 1 Pound

Mboga mchanganyiko za barafu - 1 Mug (Frozen vegetable)  

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi  - 2 vijiko vya supu

Garam masala - 1 kijiko cha supu

Nyanya - 1 

Kitungu maji - 1

Mdalasini nzima - 1 vijiti

Karafuu - 3 chembe

Pilipili mbichi  - 1

Chumvi - kiasi

Maji - 2 ½ Mugs

Mafuta - 3 vijiko vya supu

Mraba ya supu ya nyama - kidonge 1, au supu yenyewe kiasi cha kutia ladha (hakikisha supu isizidi kipimo).

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Osha mchele na uroweke kiasi kutegemea aina ya mchele.
  2. Katakata viazi kaanga katika mafuta, toa weka kando.
  3. Tia mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji mpaka kigeuke rangi ya hudhurungi (brown).    
  4. Tia nyama ya kusaga, thomu na tangawizi, pilipili, bizari zote na chumvi. Kaanga hadi nyama iwive.
  5. Katakata nyanya uliyokatakata itie katika mchanganyiko wa nyama na endelea kukaanga kidogo tu.
  6. Tia mboga ya barafu (frozen vegetables)
  7. Tia maji, kidonge cha supu au supu ya nyama kiasi tu cha kutia ladha.
  8. Yatakapochemka tia mchele.
  9. Punguza moto uwe mdogo funika kwa muda wa ½ saa hadi wali ukauke na uwive. Utakuwa tayari  kuliwa.
Share