Skip navigation.
Home kabah

Muda Wa Kurudi Katika Dini

SWALI:

Asalaam  Alaikum  Warahmatulhaahi  Wabarakaatuhu,  mimi  sijambo [ Al Hamdulillaah] kama  nanyi  hamjambo viongozi  wetu wa Dini  ya kweli basi ni kheri. Naomba msaada mnijibu

 3.Mtu  aliyesilim  kutoka kwenye Dini  ya  kweli  kisha  baada  ya  muda  fulani  akataka kurudi  anaruhusiwa?

 




JIBU:

Shukrani zote anastahiki Allah, Mola Mlezi wa viumbe vyote. Pia shukrani ni kwa ndugu zetu kwa kaka na dada zetu wanaouliza maswali na kaka yetu huyu ambaye ameuliza haya maswali takriban tisa

3.  Mtu ambaye alikuwa ni Muislamu kisha akaritadi anaweza kurudi katika Dini anapoona kuwa amefanya makosa. Na jambo hili lilitokea wakati wa Sayyidna Abu Bakar (r.a) ambapo Waarabu waliritadi na baadae wakarudi katika Dini yao ya asili. Na ni makosa makubwa sana kwa mtu kufanya kitendo hicho cha kuingia na kutoka katika Dini kwa dhihaka au istihzai. Lakini likifanywa mara nyingi litamletea matatizo makubwa sana mtu mwenyewe kwani litamuingiza katika ukafiri. Allah Anasema:

Hakika walio amini, kisha wakakufuru, kisha wakaamini, kisha wakazidi ukafiri, Mwenyezi Mungu hakuwa wa kuwaghufiria wala wa kuwaongoa njia” (4: 137).

 Wa Allaahu A'alam