Nani Muhimu Kumhudumia Katika Ugonjwa Mama Au Mke?
SW
Asalam aleikum, kuna ndugietuwa na muislam ametokezewa na matatizo ya maradhi ambayo imembidi kupelekwa hospitali kubwa na kufanyiwa operation.
Suala langu ni kua huyu bwana kutokezewa na tatizo
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu huduma anayohitajia mume katika ugonjwa wake. Uislamu haukuacha jambo lolote ila umetuelezea ili tusipate utata aina yoyote tunapokabiliana na tatizo au shida yoyote ile.
Ama kuhusu swali lako kila mmoja kati ya mama na mke wana jukumu kwa mgonjwa wao. Na hili si suala la kuteta wala kubishana kati ya hao wawili bali wanaweza kushirikiana kwa njia nzuri kwa wepesi wa mgonjwa. Kila mmoja kati
Hata baada ya hayo tuliyoyasema, Uislamu pia unatazama maslahi ya kila mmoja katika wanaadamu. Hapa hivyo, tunatazama maslahi ya mgonjwa. Haitakuwa maslahi ikiwa mama na mke watakuwa wanashindana au kuzozana, hivyo itakuwa afadhali kila mmoja wao amhudumie mgonjwa kwa mpangilio fulani. Kwa mfano, mke atamhudumia usiku na mama asubuhi au kinyume chake ili mwanzo kila mmoja apate hisia ya kuwa amemsaidia mgonjwa na mgonjwa naye apate kupona kwa njia nzuri zaidi kwa ushirikiano huo.
Tunamuomba Allaah Aliyetukuka Ampe shifaa mgonjwa na kuwepo uelewano baina ya mama na mke katika kumhudumia mgonjwa wao.
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
