Skip navigation.
Home kabah

027 - Kisomo Chake (صلى الله عليه وآله وسلم) Katika Swalah Ya Witr - Sifa Ya Swalah Ya Mtume

 

 

7-   SWALAH YA WITR

 

Alikuwa   (صلى الله عليه وآله وسلم)akisoma katika Rakaa ya mwanzo:

 

سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى

Sabbihi-sma Rabbikal A’laa

((Litakase Jina la Mola wako Mlezi Aliye juu kabisa)) [Al-A'laa 87: 19],

na katika Rakaa ya pili:

 

قُلْ يَا أَيُّهَا الْكَافِرُونَ

Qul Yaa Ayyuhal Kaafiyrun

((Sema: Enyi makafiri)) [Al-Kaafiruun 109: 6],

na katika Rakaa ya tatu.([1])

 

 

((قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ))

((Sema: Yeye Allaah ni wa Pekee)) [Al-Ikhlaasw 112: 4].

 

Mara nyingine alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akiongeza katika Rakaa ya mwisho kwa kusoma:

 

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ

 

Qul ‘auudhu bi Rabbil Falaq

((Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko)) [Al-Falaq 113: 5],

na

 

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ

Qul ‘auudhu bi Rabbin Naas

Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu)) [An-Naas 114: 6] ([2]).

 

Na mara nyingine alisoma katika Rakaa ya tatu Aayah mia kutoka katika Suratun-Nisaa [4: 176] ([3]).

 

Ama zile Rakaa mbili baada ya Witr([4]), alikuwa kaisoma ndani yake:

 

إِذَا زُلْزِلَتِ الْأَرْضُ زِلْزَالَهَا

 

Idhaa Zulzilatil Ardhu Zil-zaalahaa

((Itakapotetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake)) [Az-Zilzalah 99: 8], na

 

 

قُلْ يَا أَيُّهَا الْكَافِرُونَ

Qul Yaa Ayyuhal Kaafiruun

((Sema: Enyi makafiri)) [Al-Kaafiruun 109: 6]([5])

 

 

 





[1] An-Nasaaiy na Al-Haakim ambaye amesema ni Swahiyh.

[2] At-Tirmidhiy, Abul-'Abbaas Al-Aswam katika Hadiyth yake (Mjalada 2 Namba 117) na Al-Haakim ambaye amesema ni Swahiyh, na Adh-Dhahabiy amekubaliana naye.

[3] An-Nasaaiy na Ahmad kwa isnaad Swahiyh.

[4] Zimethibiti Rakaa mbili hizi katika Swahiyh Muslim na wengineo kama ni desturi ya Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم). Na kuthibiti kwa Rakaa mbili hizi, kunapingana na kauli yake (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Ifanyeni Swalah yenu ya mwisho usiku kuwa ni Witr)). Imepokelewa na Al-Bukhaariy na Muslim. Maulamaa wamekhitilafiana katika kuoanisha baina ya Hadiythi hizi mbili, kwa maono, fikra na mitazamo tofauti. Na hakuna hata mtazamo mmoja katika mitazamo yote hiyo ulionikinaisha. Na ni busara kuziacha Rakaa mbili hizi kwa mujibu wa amri ya Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم). Na Allaah Anajua zaidi.

Kisha nikakutana na Hadiyth Swahiyh ambayo ndani yake iko amri ya kuswali Rakaa mbili baada ya Witr. Kwa hiyo amri ya Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) imewafikiana na kitendo chake, na ikathibiti amri ya kuswali Rakaa mbili kwa watu wote. Na amri ya kwanza inaweza kuwa ni mapendekezo, hivyo basi hakuna kinachozikanusha Rakaa mbili. Hadiyth hiyo nimeiweka katika Silsilatul-Ahaadiyth Aswahiyhah (1193). Taz. Kiambatisho 7.

[5] Ahmad, Ibn Naswr na Atw-Twahaawiy (1/202), na Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan ikiwa na isnaad Hasan Swahiyh.