Kaimati (Aina Ya 3)

Kaimati (Aina Ya 3)

 

Vipimo

Unga - 2 vikombe vya chai

Hamira - 1 ½ cha chai

Samli - 1 kijiko cha chai

Maji - 1 ½ kikombe cha chai (kiasi)

Mafuta ya kukaangia - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Changanya unga  Hamira, Samli, maji, kisha  vuruga kulainisha unga hadi uwe hauna madonge na mwepesi kiasi.
  2. Funika unga uumuke. Ukiuumuka (ukifura) choma kaimati katika mafuta ya moto.
  3. Ziepue na zichuje mafuta.
  4. Weka kaimati katika bakuli au sahani kisha mwagia *Shira  zikiwa tayari.

Shira:

Sukari - 3 vikombe

Maji - 1 kikombe

Hiliki - ¼ kijiko cha chai

Arki (rose flavour) - 3-4 matone

Namna Ya Kutayarisha Shira

  1. Tia sukari na maji katika kisufuria kidogo, acha kwenye moto ichemke pole pole hadi iwe nzito ya kunata.
  2. Tia  hiliki na arki ikiwa tayari kumwagiwa juu ya kaimati, huku unavichanganya na huku shira ikipowa na kugeuka kuwa sukari kavu.

Kidokezo:

Shira ya Kaimati hizi iwe nzito ili unapochanganya na kaimati igeuke kuwa kama sukari ya visheti.

 

Share