Keki Ya Chokoleti Iliyokoza

Keki Ya Chokoleti Iliyokoza

 

Vipimo  

Maji yaliyochemka -  2 Vikombe vya chai 

Unga wa kaukau (cocoa powder) -  1 Kikombe 

Unga -  2 ¾ Vikombe 

Baking soda - 2 Vijiko vya chai 

Baking powder -  ½ Kijiko cha chai 

Chumvi -  ½ Kijiko cha chai 

Siagi iliyolainika - 1 Kikombe 

Sukari -  2 ¼ Vikombe 

Mayai -  4 

Vanilla -   1 ½ Kijiko cha chai  

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Washa oveni moto wa 350° F. Kisha paka siagi/mafuta treya ya kuchomea keki.
  2. Katika bakuli la kiasi, mimina yale maji ya moto yaliyochemka juu ya unga wa kaukau (cocoa powder), na uchanganye (kwa whisking spoon) hadi ilainike, kisha iyache ipoe.
  3. Kwenye bakuli la kiasi, chunga pamoja unga, baking soda, baking powder na chumvi na uweke kando.
  4. Katika bakuli la mashine, changanya (cream) siagi na sukari pamoja mpaka ilainike vizuri.
  5. Kisha tia yai moja baada ya jengine huku unaendelea kuchanganya, halafu tia vanilla, kisha tia mchanganyiko wa unga halafu tia ule mchanganyiko wa kaukau ulouweka kando.
  6. Mimina kwenye treya ya kuchomea keki na uvumbike (bake) kwenye oveni kwa muda wa dakika 25 – 30.
  7. Iache ipoe halafu itayarishie malai ya chokoleti (cream chocolate).   

Vipimo Vya Malai Ya Chokoleti (cream chocolate) 

Siagi -  ¼ Kikombe 

Sukari laini (icing sugar) -  1 Kikombe 

Unga wa kaukau (cocoa powder) -  1 Kijiko cha supu 

Maji ya moto -  2 Vijiko vya supu 

Namna Ya Kutayarisha  

  1. Katika bakuli la mashine, changanya vipimo vyote hadi ilainike vizuri. Unaweza kuongeza maji ikiwa mchanganyiko ni mzito sana.
  2. Kisha unapaka juu ya keki iliyopoa kwa kutumia kisu cha siagi au mwiko uliobapa (flat).
  3. Kisha tia mchanganyiko wa malai ya sukari kiasi katika mirija/nozeli (icing tube/icing nozzle) ili itoe usanifu (design) juu ya keki kama ilivo kwenye picha hapo juu au upendavyo.  Kata vipande saizi upendayo. 

 

 

 

Share