Mchicha (Swiss Chard) Na Bamia

Mchicha  (Swiss Chard) Na Bamia

  

Vipimo  

Majani ya Mchicha (Swiss Chard) - 4  - 5 

Bamia - 150 - 250g 

Chumvi - 1 kijiko cha chai 

Mafuta ya zaituni - ½  kikombe 

Maji - 1 gilasi          

Kitunguu maji kilokatwakatwa - 1  

Namna Ya Kutayraisha Na Kupika  

  1. Katakata sehemu ya juu ya majani ubakishe majani pekee. 
  2. Osha majani kisha katakata kama mchicha wa kawaida . 
  3. Tia mboga katika sufuria, maji na chumvi chemsha kwa dakika 25 hivi. 
  4. Osha bamia  uweke tayari ukiwa umezikata vikonyo vyake. 
  5. Mboga ikishachemka kurudia chini mimina bamia, kitunguu, mafuta . Acha ichemke mpaka bamia ziwive ikiwa tayari. 

Kidokezo: 

Mboga hii ni aina ya mchicha ila hatujui inaitwaje kiswahili, ila tunajua inatiwa Swiss Chard.

  

 

 

 

Share