033-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Adhkaar Za Rukuu

 

ADHKHAAR ZA RUKUU

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) katika nguzo hii akisoma namna mbali mbali za adhkaar na du'aa. Alikuwa akibadilisha katika kusoma kwake; mara nyingine husema hii na mara nyingine husema hii miongoni mwa zifuatazo:

 

1.

Sub-haana Rabbiyal ‘Adhiym

 

“Ametakasika Mola wangu Aliye Mtukufu, mara tatu”([1]). Na mara nyingine alikuwa akiikariri zaidi ya hivyo.([2]) 

 

Mara moja, katika Swalah ya usiku, aliikariri sana hadi rukuu yake ikawa inakaribiana na kisimamo chake, alichokuwa amesoma ndani yake Surah tatu katika Surah ndefu; Al-Baqarah, An-Nisaa na Al-'Imraan. Ndani yake (Swalah hii) kulijaa du'aa na kuomba Maghfirah, kama ilivvyotajwa katika '(Kisomo Katika) Swalah Ya Usiku (Tahajjud).

 

 

2.

Sub-haana Rabbiyal ‘Adhiym wabihamdihi

 

“Ametakasika Mola wangu Aliye Mtukufu Na Sifa Njema Zote Ni Zake, mara tatu”.([3])

 

 

3.

Subuuhun Qudduusun Rabbul Malaaikati war Ruuhi

 

“Mwingi wa kutakaswa Mtakatifu([4]), Mola wa Malaika na Jibriyl”.([5])

 

 

4.      

Sub-haanaka Allaahumma wa Biham-dika Allaahumma gh-fir-liy

 

“Kutakasika ni Kwako, Ee Mola wangu, na sifa njema zote ni Zako, Ee Mola Nisamehe". Alikuwa akiileta kwa wingi hii katika rukuu yake na sujuud zake, alikuwa akitekeleza amri ya Qur-aan.”([6])

 

 

5.

Allaahumma laka Raka’tu, wabika Aamantu, walaka As-lamtu, [Anta Rabbiy] Khasha’a laka sam’iy, wabaswariy, wamukh-khiy, wa’adhwmiy, [wa ‘idhwaamiy] wa’aswabiy, [wamas-taqallat bihii Qadamiy Lillaahi Rabbil ‘Alamiyn]

 

“Ee Allaah! Kwako Wewe nimerukuu, na Wewe nimekuamini, na Kwako Wewe nimejisalimisha, (Wewe Mola wangu) umenyenyekea  Kwako usikizi wangu, na uoni wangu, na ubongo wangu, na mfupa wangu, (katika riwaaya mifupa yangu) na hisia zangu, (na ambacho kimesimama juu ya miguu yangu([7]) kwa ajili ya Mola Wa viumbe vyote.”([8])

 

 

6.

Allaahumma laka Raka’tu, wabika Aamantu, walaka As-lamtu, wa’alayka tawakkaltu, Anta Rabbiy, Khasha’a laka sam’iy, wabaswariy, wadamiy, walahmiy, wa‘adhamiy, wa’aswabiy, Lillahi Rabbil ‘Alamiyn

 

“Ee Allaah! Kwako nimerukuu, na Wewe nimekuamini, na Kwako nimejisalimisha, Kwako nimekutegemea, Wewe Mola wangu,  umenyenyekea  Kwako usikizi wangu, na uoni wangu, na damu yangu, na nyama yangu, na mfupa wangu, na ubongo wangu kwa ajili ya Mola Wa viumbe vyote”.([9])

 

 

7.

Subhaana dhil Jabaruuti wal Malakuuti wal Kibriyaau wal ‘Adhamati

 

“Ametakasika Mwenye Utawala, na Ufalme, na Ukubwa, na Utukufu”, Hii alikuwa akiisoma katika Swalah ya usiku.([10])

 

 

[1] Ahmad, Abu Daawuud, Ibn Maajah, Ad-Daaraqutwniy, Atw-Twahaawiy, Al-Bazzaar na Atw-Twabaraany katika Mu'jam Al-Kabiyr, kutokana na Maswahaba saba. Ndani yake kuna jibu kwa wale waliokataa ujio wa kutozidi mara tatu katika kuleta Tasbiiyhaat, kama Ibn Al-Qayyim na wengineo.

[2] Inapatikana hii kutokana na Ahaadityh zilizoweka wazi kwamba Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akifanya kisimamo chake, na rukuu yake na sujuud zake sawa sawa kwa urefu, kama itakavyotajwa katika mlango ufuatao.

[3] Hadiyth Swahiyh. Imesimuliwa na Abu Daawuud, Ad-Daaraqutwniy, Ahmad, Atw-Twabaraaniy na Al-Bayhaqiy.

[4] Abu Is-haaq amesema: "Subuuh" ina maana ya Aliyetakasika na makosa yoyote, na "Qudduus" ina maana ya Mwenye Baraka au Aliyetwaharika". Ibn Saydah: "Subbuuh Qudduus" ni sifa za Allaah عزوجل kwa sababu Anatukuzwa na Kutakaswa". (Lisaanul-'Arab).

[5] Muslim na Abu 'Awaanah.

[6] Al-Bukhaariy na Muslim. Na maana ya “yata-awwalul Qur-aan” ni kuwa anatekeleza yale aliyoamrishwa ndani yake katika maneno Yake Allaah:

((فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَاسْتَغْفِرْهُ إِنَّهُ كَانَ تَوَّابًا)).

((Zitakase sifa za Mola wako, na umwombe msamaha, hakika Yeye Ndiye Anayepokea tawbah)) [An-Naswr 110: 3]

[7] Ina maana niliyoyabeba, kutokana na neno "al-istiqlaal" lenye maana "al-irtifaa’". Ni ujumla (ta’miym) baada ya ukhusuusi (takh-swiys), kwa maana imekuja –niliyoyabeba- baada ya khusuus -kutaja kiungo kimoja kimoja- katika viungo vya mtu).

[8]    Muslim, Abu 'Awaanah, Atw-Twahaawiy na Ad-Daaraqutwniy.

[9] An-Nasaaiy kwa isnaad Swahiyh.

  

[10]Abu Daawuud, An-Nasaaiy kwa isnaad Swahiyh. 

 

FAIDA

Je, inakubalika kuchanganya baina ya hizi adhkaar (mbili au zaidi) katika rukuu moja au haikubaliki? Maulamaa wametofautiana katika hili. Ibn al Qayyim hakuwa na msimamo kuhusu hili katika Zaad Al-Ma'aad, na An-Nawawiy amechagua uwezekano wa mwanzo katika Al-Adhkaar, akisema: "Na lililo bora ni kuchanganya baina ya hizi adhkaar zote ikiwezekana. Na hivi ndio inavyotakikana iwe katika adhkaar za milango yote. Abu Atw-Twayyib Swiddiyq Hasan Khan katika Nuzuul Al-Abraar (84) hakukubaliana naye kwa kusema: "Alete adhkaar hizi mara hii, na alete adhkaar nyingine mara nyingine, wala sioni dalili ya kuchanganya. Mjumbe wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)   hakuwa akizichanganya kwa mpigo mmoja, lakini alikuwa mara akisema hii, na mara nyingine akisema nyingineyo. Na kufuata ni bora kuliko kuzusha". (Rai ya mwisho hii ni rai iliyo sahihi,) na hivi ndio haki Insha Allaah. Lakini imethibitika katika Sunnah kuirefusha nguzo hii na nyingine pia (kurukuu huku), kama itakavyokuja ufafanuzi wake, hadi iwe inakaribia urefu wa kisimamo. Hivyo, mwenye kuswali akipenda kumfuata Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Sunnah hii, basi hatoweza kufanya hivyo, isipokuwa kwa njia ya kuzichanganya tu (adhkaar) ambayo amekwenda/ameifuata An-Nawawiy, na Ibn Naswr ameipokea katika Qiyaamul-Layl (76) kutoka Ibn Jurayj kutokana na 'Atwaa, -haitowezekana- isipokuwa kwa njia ya kukariri iliyotaja katika baadhi ya hizi adhkaar. (moja ambayo inayo maandiko ya kukariri,) na hivi ndivyo karibu na Sunnah Na Allaah Anajua zaidi.

Share