Pilau Ya Kuku

Pilau Ya Kuku

   

 

Vipimo

Mchele wa basmati - 3 vikombe

Kuku - ½

Viazi - 4

Vitunguu - 2

Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa - 2 vijiko vya supu

Binzari ya pilau nzima - 1 Kijiko cha chakula

Binzari ya pilau - ½ kijiko cha chai

Pilipili manga nzima -  ½ kijiko cha chai

Karafuu nzima - 8

Iliki nzima - 6

Mdalasini nzima - 5 vijiti

Pilipili mbichi iliyosagwa - 2

Chumvi - kiasi

Mafuta ya kupikia - ¼ kikombe

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika:

  1. Osha mchele na roweka kwa muda kutegemea na aina ya mchele.
  2. Kata kuku vipande upendavyo, safisha kisha mchemshe kwa chumvi, pilipili iliyosagwa, thomu na tangawizi.
  3. Akiwiva kuku, mtoe weka kando, bakisha supu katika sufuria.
  4. Katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangu ya hudhurungi.
  5. Tia thomu na tangawizi na binzari zote kaanga kidogo
  6. Kisha tia viazi kanga kidogo kisha tia kisha tia vipande vyako vya kuku na supu acha ichemke kidogo kisha tia maji ukisie kutokana na mchele unaotumia.
  7. Mwisho tia mchele koroga uchanganye na vitu vyote acha ichemke kiasi kisha funika na punguza moto mpaka uive (huku ukiugeuzageuza)
  8. Ukishakuwa tayari pakua  kwenye sahani tayari kwa kula na salad na pilipili.

 

 

Share