Skip to main content

Kutoa Zakaah (Zakaatul-Maal)004-Kutoa Zakaah: Kufaradhishwa Zakaah

Kutoa Zakaah: Kufaradhishwa Zakaah

Alhidaaya.com

Zakaah imefaradhishwa wakati Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa Makkah katika siku za mwanzo za Uislaam, lakini hapakuwekwa Nisaab, (kiwango cha mali ambacho mtu akiwa nacho kwa muda wa mwaka analazimika kuitolea Zakaah), wala kiasi cha kulipa, isipokuwa waliachiwa Waislam wenyewe kukisia kiasi cha kutoa.

Katika mwaka wa Pili baada ya Hijrah, ilifaradhishwa kiasi chake katika kila aina ya mali na kubainishwa vizuri.