017-Kutoa Zakaah: Kuomba Du’aa

 

Kutoa Zakaah: Kuomba Du’aa

 

Alhidaaya.com

 

Inapendeza kumuombea dua mtoaji Zakaah, pale anapoitoa.

 

Allaah Anasema:

خُذْ مِنْ أَمْوَالِهِمْ صَدَقَةً تُطَهِّرُهُمْ وَتُزَكِّيهِم بِهَا وَصَلِّ عَلَيْهِمْ إِنَّ صَلاَتَكَ سَكَنٌ لَّهُمْ

Chukua (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) katika mali zao Swadaqah, uwatakase na ziwazidishie kwazo na waombee du’aa (na maghfirah). Hakika du’aa yako ni utulivu kwao. [At-Tawbah: 103]

 

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Abi ‘Awfiy amesema:

 

“Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapoletewa mali ya Zakaah akisema: "Allaahumma swalliy ‘alayhim". Na baba yangu siku moja alimpelekea mali ya Zakaah akasema: "Allaahumma swalliy ‘alaa aali Abi ‘Awfiy". [Ahmad na wengineo].

 

Imepokelewa kutoka kwa Waail bin Hujr kuwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimuombea mtu mmoja aliyeleta ngamia wa Zakaah akasema:

 

"Allaahumma Baarik fiyhi wa fiy ibilihi". (Allaah mbariki yeye na katika ngamia wake)

 

Anasema Imaam Ash-Shaafi’iy:

 

"Ni Sunnah kwa Imaam anapopokea mali ya Zakaah kumuombea dua mtoaji kwa kumwambia: "Aajaraka Allaahu fiyma a’atwayta, wa baarik laka fiyma abqayta".

 

(Allaah akupe ujira mwema katika ulichotoa na akubarikie katika kilichobaki).

 

Share