Skip navigation.
Home kabah

Kulala Na Janaba Na Kuamka Na Swawm

SWALI: 

asalam aleikum

swala langu ni ikiwa mtu amelala na janaba siku ya ramadhan  akamka asubuhi  je saum ina swih ama itakuwa haifai

 

 


JIBU:

AlhamduliLLah,  Waswalaatu Was-salaam 'alaa Rasuli-Llah  صلى الله عليه وآله وسلم Amma ba'ad,

 Jibu ni kwamba inafaa kulala na janaba na kuamka kutia Twaharah (ghuslu) asubuhi lakini   kabla ya jua kuchomoza ili uwahi kuswali swalah ya Alfajiri na Swawm yako itaswihi.

Tazama pia Swali na Jibu katika kitengu hiki kifuatacho kuhusu maudhuu hiyo. 

Wakati Wa Mwisho Kukoga Janaba Katika Mwezi Wa Ramadhaan

Na Allaah Anajua Zaidi