Wazinifu Waliotubu Wanaweza Kufunga Ndoa Na Waliotakasika





SWALI

 

(Nimeona nakala ilitumwa katika moja ya sites za Kiswahili

muandikaji katika kujibu nakala za mwengine alitoa hoja kuwa,

Mtume  SAW alipokuja kuwaleta watu katika haki na kuacha machafu, hajawaamrisha wale walioowana kabla ya Uislam waowane kwa mara ya pili, na pia aliuliza kama kuna hadithi au Aya ambayo jambo kama hili lilitokezea wakati wa Mtume SAW nae Mtume  akawaambia watu wavunje ndoa yao kwasababu walizini kabla ya hapo, na hoja nyingi alizitoa muandikaji kwa

kusema jee kwa wakati wa leo watu kama watasilimu hali ya wao walioana kabla jee waozeshwe tena? na alipokuwa akijibu hoja iliyotolewa katika Aya MZINIFU HAOI ISIPOKUWA KWA MZINIFU MWENZIWE NA HILO  NI HARAMU, alisema hii inaonyesha kuwa kama mtu alikuwa mzinifu asipewe mtoto alikuwa msafi (asiekuwa mzinifu) kumuoa, na wala wale wasiozini

wanaume wasioe wazinifu wanawake, sasa hapa tunaomba tuwekwe sawa
 maana katika hiyo hiyo Aya inaishia kusema na jambo hilo ni haramu. Sasa  hawa watu kama wameamua kutubia na kurudi kwa Mola wao kihaki lilah na wakaoana patakua uharamu wowote? Tafadhali msione dhiki kujibu masuali yetu ndio kutaka kujua kwa usahihi. Na naomba Mnapotujibu katika

maelezo mengi na mkiishia muweke japo mstaari mmoja kuwa hili jambo ni linafaa au halifai kisheria.

 



 

JIBU:

Kwa mafunzo sahihi   kwa mujibu wa itikadi ya Salafus Swaalih (wema waliopita) ambayo ndio Itikadi ya Ahlus Sunnah wal Jama'ah, wanamzingatia mwenye kufanya madhambi makubwa kama ni mwasi au fasiki. Na vile vile  wenye kufa hali ya kuwa anatenda madhambi makubwa, basi mtu huyo yupo katika mapendeleo ya Mwenyeezi Mungu. Akitaka Atamsamehe kwa ukarimu Wake na Akitaka Atamwadhibu kwa uadilifu Wake mpaka atakasike na makosa ya uasi wake kisha atahamia peponi. Ama itikadi ya wengine kama Makhaawarij, wao   humwiita mwenye kufanya madhambi makubwa  kafiri wakidai kwamba huu ni ukafiri wa neema au ukafiri wa unafiki, si ukafiri wa dini, na pia  wanasema kwamba mwenye kufanya maasia, basi huyo ni mtu wa motoni milele.

 

Kwa hiyo Muislamu aliyetubu kikweli  kutokana na   kitendo cha zinaa,  akafuata shuruti za Tawbah ikawa Tawbatun-Nasuuha na akazidisha na kuendelea kufanya vitendo vyema badili yake, basi  alama ya zinaa huondoka, yaani haitwi tena mzinifu, bali  husamehewa kama yule aliyefanya matendo ya shirki, kuua ambayo ni maasi yenye madhambi makubwa kama ilivyo zinaa. Mwenyeezi Mungu Anasema:

}}وَالَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ اللَّهِ إِلَهًا آخَرَ وَلَا يَقْتُلُونَ النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّهُ إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَا يَزْنُونَ وَمَن يَفْعَلْ   ذَلِكَ يَلْقَ أَثَامًا{{

 

}}يُضَاعَفْ لَهُ الْعَذَابُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَيَخْلُدْ فِيهِ مُهَانًا{{

 

}}إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ عَمَلًا صَالِحًا فَأُوْلَئِكَ يُبَدِّلُ اللَّهُ سَيِّئَاتِهِمْ حَسَنَاتٍ وَكَانَ اللَّهُ غَفُورًا رَّحِيمًا{{

 {{ Wale wasio mwomba mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu,  wala hawaui nafsi aliyo iharimisha Mwenyezi Mungu isipo kuwa kwa  haki, wala hawazini - na atakaye fanya hayo atapata madhara}}

{{azidishiwa adhabu Siku ya Kiyama, na atadumu humo kwa kufedheheka}}

{{Isipokuwa atakaye tubu, na akaamini, na akatenda vitendo vyema.  Basi hao Mwenyezi Mungu atayabadilisha maovu yao yawe mema.  Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu}}

Al-Furqaan: 68-70

Hadithi hii hapa chini pia inathibitisha kusamehewa huko kwa vitendo kama hivyo:

 ((عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا أَنَّ نَاسًا مِنْ أَهْلِ الشِّرْكِ كَانُوا قَدْ قَتَلُوا وَأَكْثَرُوا وَزَنَوْا وَأَكْثَرُوا ، فَأَتَوْا مُحَمَّدًا صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ، فَقَالُوا : إِنَّ الَّذِي  تَقُولُ وَتَدْعُو إِلَيْهِ لَحَسَنٌ ، لَوْ تُخْبِرُنَا أَنَّ لِمَا عَمِلْنَا كَفَّارَةً ، فَنَزَلت:      

 

}}والذينَ لا يَدْعُونَ مَعَ اللَّهِ إِلَهًا آخَرَ وَلا يَقْتُلُونَ النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّهُ إِلا بِالْحَقِّ وَلا يَزْنُونَ {{ وَنَزَلَتْ :   }} قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَى أَنْفُسِهِمْ لا تَقْنَطُوا مِنْ رَحْمَةِ اللَّهِ{{   ))

 

  روى البخاري (4436) ومسلم (174)

 

((Imetoka kwa Ibn 'Abbaas رضي الله عنهما ambaye kasema;  baadhi ya watu Mushrikiin ambao waliua sana na kutenda zinaa  kwa wingi walikuja kwa Mtume صلى

 الله عليه وآله وسلم  na kumwambia; Unayotuitia (katika Uislamu) ni mazuri, lakini tujulishe tu kama kuna kafara ya yale maovu tuliyoyafanya;  hapo zikateremshwa  aya hizi:   

{{Na wale wasio mwomba mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu, wala hawaui nafsi aliyo iharimisha Mwenyezi  Mungu isipo kuwa kwa haki, wala hawazini} Al-Furqaan: 68

Na ikateremka:

{{Sema: Enyi waja wangu walio jidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu}}))     Az-Zumar: 53  (Al-Bukhari na Muslim)

Kisha baada ya kutubu anatakiwa Muislamu ajistiri kwa kuficha  siri yake ya mambo aliyofanya maovu kabla, na sio kujifehedhesha kwa kuyatangaza maovu hayo na kujisifu nayo, kama livyotuambia  Mtume صلى الله عليه وآله وسلم   katika hadithi hii  :  

 (( اجتنبوا هذه القاذورة التي نهى الله عز وجل عنها ، فمن ألم فليستتر بستر الله عزوجل))  رواه البيهقي وصححه الألباني في السلسلة الصحيحة 663 

 

((Jiepusheni  na uchafu huu alioukataa Allaah عزوجل, na atakaye tenda dhambi ya aina hiyo, basi ajisitiri kwa stara ya Allaah   ((عزوجل

[Al-Bayhaaqiy na Amesahihisha Saykh Al-Albaaniy katika Silsilatus Swahiyhah: 663.]

 

Kwa hivyo suali lako kuhusu Aaya katika Suratun-Nuur

}}الزَّانِي لَا يَنكِحُ إلَّا زَانِيَةً أَوْ مُشْرِكَةً وَالزَّانِيَةُ لَا يَنكِحُهَا إِلَّا زَانٍ أَوْ مُشْرِكٌ وَحُرِّمَ ذَلِكَ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ{{ 

{{Mwanamume mzinifu hamwoi ila mwanamke mzinifu au mwanamke mshirikina. Na mwanamke mzinifu haolewi ila na mwanamume mzinifu au mshirikina. Na hayo yameharimishwa kwa Waumini.}} An Nuur:3

inakusudiwa wale ambao bado wanaendelea katika katika kitendo hicho cha zinaa. Ama waliotubu kikweli wanaweza kuoa na kuolewa na waliotakasika.

Kama ulivyotaka tujibu kwa kifupi mwisho, ni kwamba "Baada ya kutubia Tawbah ya kweli ndoa itasihi na inafaa ndoa na waliotakasika"   

 

Wa Allaahu A'alam 

 

 

Share