03-Tawbah Hukmu Na Fadhila Zake: Tawbah Ya Naswuwhaa (Ya Kwelikweli) Na Masharti Yake

Tawbah Hukmu Na Fadhila Zake

 

03-Tawbah Ya Naswuwhaa Kweli Na Masharti Yake

 

 

 

Kuomba maghfirah na tawbah, kunampasa Muumini awe na yaqini kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Atamghufuria madhambi madhambi yake pindi yakitimizwa masharti yake. Na kufanya hivyo ndio inapohakiki Tawbah ya Naswuwhaa (Tawbah ya kikwelikweli). Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ametuamrisha tuiombe tawbah hiyo Anaposema:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا تُوبُوا إِلَى اللَّـهِ تَوْبَةً نَّصُوحًا

Enyi walioamini! Tubieni kwa Allaah tawbah ya nasuha (kwelikweli) [At-Tahriym: 8]   

 

 

Tawbah Ya Naswuwhaa (Tawbah ya kwelikweli) ni kutubia kikweli kwa kuijiepusha na maasi yote, na kujirekebisha kwa kutokurudia hayo maasi aliyokuwa akiyatenda Muislamu na badili yake mtu azidishe kufanya mema. Na anapoomba mtu Tawbah ya kweli bila shaka Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Atamghufuria madhambi yake zote. Anasema Allaah:

 

 وَإِنِّي لَغَفَّارٌ لِّمَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا ثُمَّ اهْتَدَىٰ ﴿٨٢﴾

 Na hakika Mimi bila shaka ni Mwingi mno wa kughufuria kwa anayetubia na akaamini na akatenda mema kisha akaendelea kuongoka.  [Twaahaa: 82]

 

Masharti Ya Tawbah Ya Naswuwhaa:

 

Zifuatazo ni shuruti za Tawbah Ya Naswuwhaa:  

 

1.     Kuomba maghfirah  

2.     Kuacha hayo maasi

3.     Kujuta

4.     Kuweka niyyah (azimio) kutokurudia tena maasi hayo.

5.     Kama kaidhulumu haki ya mtu basi ni kuirudisha hiyo haki.  

 

 

 

 

Share