Sphagetti Kwa Sosi Ya Fasulia (Maharage Machanga) Na Kabaab Za Kukaanga

Sphagetti Kwa Sosi Ya Fasulia Na Kabaab Za Kukaanga

 

 

Vipimo

 

Sphagetti - 1 paketi

 

Vipimo vya Kababu

Nyama ya kusaga - ½ kilo

Tangawizi mbichi ilosagwa - 2 vijiko vya kulia

Bizari mchanganyiko - 1 kijiko cha kulia

Pilipili mbichi ya kijani ilosagwa - 2-3

Chumvi - kiasi

Kotmiri katakata - kiasi

Mayai - 2

Slesi ya mkate - 4-5

Mafuta ya kukaangia

 

Vipimo Vya Sosi

 

Fasulia (maharage meupe machanga) - 1 kikombe

Kitunguu kilokatwakatwa - 2

Nyanya zilokatwakatwa - 3

Nyanya ya paste – tomatoe paste - 3 vijiko vya kulia

Pilipili boga la kijani - 1

Herbs: Nanaa kavu, organo, zaatari - ½ kijiko cha chai kila moja

Mafuta - kiasi

 

 Namna Ya Kutayarisha Na Kupika  

 Kabaab:

  1. Roweka slesi za mkate katika bakuli dogo, kamua maji na chuja.
  2. Katika bakuli changanya vitu vya kabaab pamoja na mkate ulokamua.
  3. Fanya duara anza kukaanga moja kwanza, ukiona haishiki, ongezea unga wa dengu kijiko kimoja cha kulia.
  4. Kaanga katika mafuta kwenye karai.

Sosi Ya Fasulia

  1. Roweka fasulia (maharage machanga) kisha chemsha yawive.
  2. Weka mafuta katika sufuria, kaanga vitunguu mpaka vianze kugeuka rangi.
  3. Tia nyanya kaanga ziive kisha tia nyanya paste na vitu vingineyo kaanga kidogo.
  4. Changanya na fasulia sosi ikiwa tayari.
  5. Chemsha sphagetti, tia mafuta kidogo unapochemsha.
  6. Mwaga maji uchuje kisha pakua katika chombo.
  7. Pakua kwenye sahani sphagetti, mwagia sosi ya fasulia na weka kabaab juu yake.  

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)

 

 

Share