29-Wewe Pekee Tunakuabudu: Tawassul Za Shirki Kufru Na Bid’ah: Kutawassal Kwa Du’aa Ya "Al-Jawshan Al-Kabiyr"

 

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ

Wewe Pekee Tunakuabudu Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada

 

Tawassul Za Shirki Kufru Na Bid’ah

 

29-Kutawassal Kwa Du’aa Ya  "Al-Jawshan Al-Kabiyr"

 

 

 

 

Al-Jawshan Al-Kabiyr (Diraya Kubwa) الجوشن الكبير

 

 

Hii ni du’aa ya uzushi na iliyojaa uongo.  Inadai yafuatayo:

 

 

a)Jibriyl alimshukia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa katika vita akiwa na jawshan (diraya - vazi la kiaskari kama kizibao cha ngozi ngumu au chuma) akasema: Ee Muhammad, Rabb wako Anakupa salamu, Anakwambia vua hilo al-jawshan, na soma du’aa hii, kwani hiyo ni amani kwako na umma wako.”

 

 

b) “Atakayeiandika katika kafani yake, Allaah Atastahi kumuadhibu na moto. Na Atakayeiomba kwa nia safi mwanzo wa mwezi wa Ramadhwaan, Allaah Atamruzuku usiku wa Layalatul-Qadr, na Atamuumbia Malaika elfu sabiini wanamsabbih Allaah, na wanamtukuza, na Atajaalia thawabu zao kwake. Na atakayeomba katika mwezi wa Ramadhwaan mara tatu, Allaah Ataharamisha mwili wake dhidi ya moto, na atawajibika Pepo, na Allaah Atamwakilishia Malaika wawili wamhifadhi na maasi, na atakuwa katika amani ya Allaah uhai wake wote.”

 

 

c) “Al-Husayn amesema: ameniusia baba yangu ‘Aliy bin Abiy Twaalib kuhifadhi du’aa hii, na kuitukuza, na kuiandika katika kafani yake, na niwafundishe ahli yangu, na niwahimize nayo, nayo ni majina elfu na humo mna jina tukufu kabisa.”.

 

 

d) “Yeyote atakayeisoma na kuibeba (kuifanyia hirizi) anapotoka nyumbani kwake wakati wa Swalaah ya Alfajiri au Swalaah ya ‘Ishaa, itakuwa kama amefanya vitendo vikubwa vyema na kama kwamba amesoma Tawraat, Injiyl na Zabuwr na Qur-aan.”

 

 

Haya yamezidi uongo kwani hakuna kilicho sawa na vitabu vya Allaah! 

 

 

e) “Allaah Atampa kwa kila herufi asomayo, wake wawili wa huwrul’ayn (wanawake wa Peponi wenye macho mazuri) na Atamjengea kasri Peponi na Allaah Atampa thawabu kama hizo za Manabii wane; Ibraahiym, Muwsa, ‘Iysa na Muhammad.”

 

Huu ni uongo wa dhahiri kwani thawabu za Mitume hazipati yeyote ila wenyewe! 

 

 

f) “Allaah Atampa thawabu sawa na jini dume na jike la miongoni mwa majini walioamini tokea siku Aliyowaumba hadi siku ya kufufuliwa na Allaah Atampa thawabu za mashuhadaa 900,000.”.

 

 

g) “Du’aa hii ina manufaa kupata mapenzi na kufaulu kuondosha fundo za ndimi, kukabiliana na mahakimu, maamiri na wafalme na kuepusha mbali silaha zote za vyuma na risasi na kukidhia  haja n.k.”

 

 

Lililo dhahiri kwamba du’aa hiyo imejaa kauli za uongo za kila aina, na imejaa madai ya fadhila na mahadhi. Na la ajabu zaidi ni kwamba du’aa hiyo ni ndefu mno kupita kiasi kufikia idadi ya nukta mia (100) za hiyo duaa! 

 

Hili si jambo la kawaida abadani katika du’aa za Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa sababu aghlabu ya du’aa zake ni fupi zenye mkusanyiko wa maneno kwa dalili:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  قَالَ:  ((فُضِّلْتُ عَلَى الأَنْبِيَاءِ بِسِتٍّ:  أُعْطِيتُ جَوَامِعَ الْكَلِمِ، وَنُصِرْتُ بِالرُّعْبِ، وَأُحِلَّتْ لِيَ الْغَنَائِمُ، وَجُعِلَتْ لِيَ الأَرْضُ طَهُورًا وَمَسْجِدًا، وَأُرْسِلْتُ إِلَى الْخَلْقِ كَافَّةً، وَخُتِمَ بِيَ النَّبِيُّونَ))

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraryah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Nimefadhilishwa juu ya Manabii kwa mambo sita; nimepewa ‘Jawaami’ul-Kalimi’ (Mjumuisho wa maana nyingi katika maneno machache) na nimenusuriwa kwa [kutiwa] hofu [katika nyoyo za maadui] na nimehalalishiwa ghanima  na nimefanyiwa ardhi kuwa kitoharishi na masjid [mahali pa kuswali], na nimetumwa kwa viumbe wote, na Manabii wamekhitimishwa kwangu)) [Muslim]

 

Na pia kama alivyosimulia ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa):

 "كَانَ رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه وسلم) يَسْتَحِبُّ الْجَوَامِعَ مِنَ الدُّعَاءِ، وَيَدَعُ مَا سِوَى ذَلِكَ".

“Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akistahabu du’aa za ujumla na akiacha zisizokuwa kama hizo.” [Abu Daawuwd na Ameipa daraja ya Swahiyh Shaykh Al-Baaniy]

 

Kauli yake: “Akistahabu du’aa za ujumla.” Ina maana; zinazojumuisha malengo mema na makusudio sahihi au zinazojumuisha thanaa kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na adabu za mas-ala. Na kauli yake. “Akiacha zisizokuwa kama hizo.” Amekusudia du’aa ndefu na ambazo hazijumuishi malengo sahihi.” [Sharh Sunan Abu Daawuwd 5/397-398 na katika ‘Awnil-Ma’buwd 4/249] 

 

Kauli yake: “Za ujumla.” Ina maana; kheri za dunia na Aakhirah na hiyo kwa lafdhi ya uchache. Maana yake, wingi, kama kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الْآخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ ﴿٢٠١﴾

Na miongoni mwao kuna wasemao: “Rabb wetu Tupe katika dunia mazuri na katika Aakhirah mazuri na Tukinge na adhabu ya moto.” [Al-Baqarah: 201]

  

 

Na mfano wa du’aa za afya duniani na Akhera.” [Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah lil-Buhuuth Al-‘Ilmiyyah wal-Iftaa (23/239)]  

 

 

Du’aa hiyo imo katika vitabu vya Mashia.  Imesimuliwa katika vitabu vyao kwa isnadi iliyotungwa na kubuniwa.    Miongoni mwa hivyo vitabu vya Mashia vyenye du’aa hiyo ni kile kiitwacho: ‘Mafaatiyhul Jinaan.’ Na katika mambo Mashia wanayoyafanya wanaposoma du’aa hiyo ni kuweka Misahafu vichwani mwao wanapofika maeneo fulani kwenye du’aa hiyo! Basi hebu tanabahi ee ndugu Muislamu ujahili kama huo na vituko kama hivyo kisha jiulize na fanya utafiti kama utakuta hayo kuwa ni katika mafunzo ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake. Hakika ni uvukaji mipaka wa uzushi!

 

 

Anasema Shaykh Al-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah): “Huwezi kukuta mongoni mwa makundi yanayodai ni katika watu wa Qiblah (Waislam) walio na ujahili mkubwa kuliko Mashia (Raafidhwah), na hakuna waipendao dunia kama wao, na nimewatafiti na kuona kuwa aibu na kasoro zote wanazowasingizia nazo Maswahaba, basi wao ndio waliojawa nazo kuliko kiumbe chochote, na Maswahaba wametakasika kabisa na hayo. Hakuna shaka yoyote ile kuwa hakuna watu waongo kupita kiasi kama wao (Mashia). Ni kama yule Musaylamah al-Kadh-dhaab ambaye alidai: “Mimi ni Mtume mkweli, na Muhammad ni muongo!” Ndio kama Mashia wanaojisifu na kujitukuza kwa imani na wakiwatuhumu Maswahaba kuwa ni wanafiki, bali wao Mashia ndio katika kundi lenye unafiki mkubwa kuliko makundi yote. Na hakika Maswahaba ndio viumbe vyenye Iymaan kubwa kabisa” [Minhaajus Sunnah An-Nabawiyyah, mj. 2, uk. 87]

 

 

Tahadhari ee ndugu Muislamu na du’aa hiyo ambayo nukuu yake inaanza  kama ifuatavyo:

 

 

 

(1) اَللّـهُمَّ اِنّي اَسْأَلُكَ بِاسْمِكَ يا اَللهُ يا رَحْمنُ يا رَحيمُ يا كَريمُ يا مُقيمُ يا عَظيمُ يا قَديمُ يا عَليمُ يا حَليمُ يا حَكيمُ سُبْحانَكَ يا لا اِلـهَ إلاّ اَنْتَ الْغَوْثَ الْغَوْثَ خَلِّصْنا مِنَ النّارِ يا رَبِّ

 

(2) يا سَيِّدَ السّاداتِ يا مُجيبَ الدَّعَواتِ يا رافِعَ الدَّرَجاتِ يا وَلِيَّ الْحَسَناتِ يا غافِرَ الْخَطيئاتِ يا مُعْطِيَ الْمَسْأَلاتِ يا قابِلَ التَّوْباتِ يا سامِعَ الاْصْواتِ يا عالِمَ الْخَفِيّاتِ يا دافِعَ الْبَلِيّاتِ

 

(3) يا خَيْرَ الْغافِرينَ يا خَيْرَ الْفاتِحينَ يا خَيْرَ النّاصِرينَ يا خَيْرَ الْحاكِمينَ يا خَيْرَ الرّازِقينَ يا خَيْرَ الْوارِثينَ يا خَيْرَ الْحامِدينَ يا خَيْرَ الذّاكِرينَ يا خَيْرَ الْمُنْزِلينَ يا خَيْرَ الْمحْسِنينَ

 

(4) يا مَنْ لَهُ الْعِزَّةُ وَالْجَمالُ يا مَنْ لَهُ الْقُدْرَةُ وَالْكَمالُ يا مَنْ لَهُ الْمُلْكُ وَالْجَلالُ يا مَنْ هُوَ الْكَبيرُ الْمُتَعالُ يا مُنْشِىءَ الْسَّحابِ الثِّقالِ يا مَنْ هُوَ شَديدُ الْمحالِ يا مَنْ هُوَ سَريعُ الْحِسابِ يا مَنْ هُوَ شَديدُ الْعِقابِ يا مَنْ عِنْدَهُ حُسْنُ الثَّوابِ يا مَنْ عِنْدَهُ اُمُّ الْكِتابِ

 

(5) اَللّـهُمَّ اِنّي اَسْأَلُكَ بِاسْمِكَ يا حَنّانُ يا مَنّانُ يا دَيّانُ يا بُرْهانُ يا سُلْطانُ يا رِضْوانُ يا غُفْرانُ يا سُبْحانُ يا مُسْتَعانُ يا ذَا الْمَنِّ وَالْبَيانِ

 

(6) يا مَنْ تَواضَعَ كُلُّ شَيْءٍ لِعَظَمَتِهِ يا مَنِ اسْتَسْلَمَ كُلُّ شَيْءٍ لِقُدْرَتِهِ يا مَنْ ذَلَّ كُلُّ شَيْءٍ لِعِزَّتِهِ يا مَنْ خَضَعَ كُلُّ شَيْءٍ لِهَيْبَتِهِ يا مَنِ انْقادَ كُلُّ شَيْءٍ مِنْ خَشْيَتِهِ يا مَنْ تَشَقَّقَتِ الْجِبالُ مِنْ مَخافَتِهِ يا مَنْ قامَتِ السَّماواتُ بِاَمْرِهِ يا مَنِ اسْتَقَرَّتِ الاْرَضُونَ بِاِذْنِهِ يا مَنْ يُسَبِّحُ الرَّعْدُ بِحَمْدِهِ يا مَنْ لا يَعْتَدي عَلى اَهْلِ مَمْلَكَتِهِ

(7) يا غافِرَ الْخَطايا يا كاشِفَ الْبَلايا يا مُنْتَهَى الرَّجايا يا مُجْزِلَ الْعَطايا يا واهِبَ الْهَدايا يا رازِقَ الْبَرايا يا قاضِيَ الْمَنايا يا سامِعَ الشَّكايا يا باعِثَ الْبَرايا يا مُطْلِقَ الأُسارى

 

 

 

Share