54-Kitaab At-Tawhiyd: Asiseme Mtu “Mja Wangu”, “Mjakazi Wangu”

Mlango Wa 54

بَابٌ لا يَقُولُ عَبْدِي وَأَمَتِي

Asiseme Mtu “Mja Wangu”, “Mjakazi Wangu


 

 

فِي اَلصَّحِيحِ عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لاَ يَقُلْ أَحَدُكُمْ: أَطْعِمْ رَبَّكَ وَضِّئْ رَبَّكَ وَلْيَقُلْ سَيِّدِي وَمَوْلايَ وَلا يَقُلْ أَحَدُكُمْ: عَبْدِي وَأَمَتِي، وَلْيَقُلْ فَتَايَ وَفَتَاتِي َغُلامِي))

Katika Swahiyh (Al-Bukhaariy) kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Asiseme mmoja wenu: Mlishe Rabbaka [Rabb wako]. Mtawadhishe Rabbaka, bali aseme: Sayyidiy au Mawlaayi [Bwana wangu][1] Na asiseme mtu: ‘Abdiy au Amatiy [mjakazi wangu], bali aseme: Fataay, na Fataatiy [kijana wangu] na ghulaamiy [mvulana wangu])) [Al-Bukhaariy]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Kukatazwa kusema: "Mtumwa wangu" au "mjakazi wangu.”

 

2-Mtumwa asiseme: "Rabb wangu” wala asiambiwe: "Mlishe Rabb wako.”

 

3-Kumfundisha bwana aseme badala ya hayo: "kijana wangu” “ee bint”, “ee mvulana”

 

4-Kumfundisha mtumwa kusema badala ya hayo: “sayyidiy” au “bwana wangu.”

 

5-La muhimu hapa ni kufafanua Tawhiyd kwa ukamilifu, hata kama ni katika maneno, majina na istilahi.

 

 

 

 

[1] Mfano aseme mtu: Mlishe bwana wako badala ya kutaja Rabbaka n.k.

 

 

 

Share