009-Swahiyh Twibbin-Nabawiy: Mwongozo Wa Nabiy Katika Kiasi Cha Kula Na Kunywa

 

Swahiyh Twibbin Nabawiy

 

009-Mwongozo Wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)

Katika Kiasi Cha Kula Na Kunywa

 

 

 

Imaam Ahmad katika “Al-Musnad”[1] na wengineo, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

((مَا مَلأَ آدَمِيٌّ وِعَاءً شَرًّا مِنْ بَطْنٍ حَسْبُ ابنِ آدمَ لُقَيْمَاتٌ يُقِمْنَ صُلْبَهُ فَإِنْ كانَ لاَ بُدَّ فاعِلاً فَثُلُثٌ لِطَعَامِهِ وَثُلُثٌ لِشَرَابِهِ وَثُلُثٌ لِنَفَسِهِ))  

“Mwanadamu hajapata kujaza chombo kibaya kuliko tumbo. Yamtosha mwanadamu vitonge vya kuunyoosha uti wake wa mgongo.[2] Na ikiwa yampasa kufanya hivyo; basi theluthi moja ni ya chakula chake, na theluthi moja ya kinywaji chake na theluthi ya nafsi yake.”[3]

 

 

 

 

 

[1] Imaam Ahmad (3/132), na At-Tirmidhiy amepokea (2380), na Ibn Maajah (3349) kutoka katika Hadiyth ya Al-Miqdaam bin Ma’ad Yakrib (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ikiwa ni marfuw’an. Nimesema: Isnaad yake ni Swahiyh, na nimeweka fasli maalum katika kitabu changu: “Iyqaadhw Al-Himam Al-muntaqaa Min Jaami’ Al-‘Uluwm Wal-Hikam.” (uk 611-612)

 

[2]Yaani mgongo wake; na makusudio ni kiwiliwili kizima. Hadiyth hii tukufu inathibitisha kuwa mwana Aadam anakula ili apate kuishi, haishi ili apate kula; ikiwa lengo ni lile la kwanza; basi atakinaika kwa chakula kwa kitakachomtocheleza katika hilo; na hawezi kufikia katika hali ya kushiba, na mtu kama huyu hatonenepa kwa kuwa na mafuta mengi. Ama Yule aliye katika hali ya pili; huyu atakula na hatashiba; mfano wake ni kama vile hayawani:

يَتَمَتَّعُونَ وَيَأْكُلُونَ كَمَا تَأْكُلُ الْأَنْعَامُ  

Wanastarehe na wanakula kama walavyo wanyama wa mifugo. [Muhammad: 12]

 

[3] Hadiyth hii ni Hadiyth ya msingi katika tiba yote, na pindi tabibu Ibn Maaswiyyah alipoithibitisha alisema: “Lau watu wangetumia maneno haya basi wangesalimika na maradhi na maduka ya dawa yangefungwa.” Kwa hakika alisema hivyo; kwa sababu asili ya kila ugonjwa ni kuvimbiwa, na ndio iliyomfanya tabibu Al-Haarith bin Al-Kaladah: “Al-Himyah ni kichwa cha dawa na Al-Batwnah ni kichwa cha dawa.” Amesema vile vile, “Aliyeuwa mtu, na kumuangamiza samba porini; ni kule kuingiza chakula juu ya chakula kingine kabla hakijasagika.”

 

Haya ni baadhi ya manufaa ya kupunguza chakula, na kuacha kujaza chakula kwa lengo la ustawi wa kiwiliwili na afya yake. Ama manufaa yake kuhusu moyo na ustawi wake; kupunguza chakula kunatengeneza nyoyo na unaongeza ufahamu na kukata nafsi, kudhoofisha matamanio, ghadhabu, na wingi wa chakula hupelekea kinyume chake; amesema hilo Imaam Ibn Rajab Al-Hanbaliy (Rahimahu Allaah) katika: Jaami’ Al-‘Uluwm wal-Hikam  (2:525-526).

 

 

Share