Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Hajj: Masharti Ya Udhwhiyah Ni Yepi?

Masharti Ya Udhwhiyah Ni Yepi?

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Ni yepi masharti ya Udhwhiyah (Kuchinja kwa ajili ya 'Iyd Al-Adhw-haa)?

 

 

JIBU:

 

1-Awe mnyama wa mifugo nao ni ngamia, ng’ombe na kondoo (au mbuzi).

 

2-Afikie umri unaokubalika ki-Shariy’ah:

 

  • Kondoo miezi sita
  • Mbuzi mwaka mmoja
  • Ng’ombe miaka miwili
  • Ngamia miaka tano

 

3-Asiwe mnyama mwenye kasoro yoyote ile katika mwili wake kama vile:

 

  • Asiwe mwenye jicho lenye ubovu (chongo, jeupe weupe wa upofu) lenye kudhihirika.
  • Asiwe mgonjwa mwenye kudhihirika ugonjwa wake.
  • Asiwe kilema mwenye kudhihirika kilema chake (akawa anashindwa kutembea kawaida).
  • Asiwe aliyedhoofika, gofu, asiyechaguliwa (asiyetakiwa).

 

[Majmuw’ Al-Fataawaa (12/25)]

 

 

Share