42-Fadhila Za Laa Ilaaha Illa-Allaah: Amsaynaa Wa Amsal-Mulku LiLLaah WalhamduliLLaah Laa Ilaaha Illa-Allaah…Miongoni Mwa Adhkaar Za Asubuhi Na Jioni.

 Hadiyth Kuhusu Fadhila Za Laa Ilaaha Illa Allaah

 

www.alhidaaya.com

 

42-Amsaynaa Wa-amsal-Mulku LiLLaah WalhamduliLLaah Laa Ilaaha Illa-Allaah

Miongoni Mwa Adhkaar Za Asubuhi Na Jioni.

 

عَنْ عَبْدِ اللهِ بِنْ مَسْعُود رضي الله عنه، قَالَ: كَانَ نَبِيُّ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم إِذَا أَمْسَى قَالَ: ((أَمْسَيْنَا وَأَمْسَى الْمُلْكُ لِلَّهِ وَالْحَمْدُ لِلَّهِ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ))‏ قَالَ: أُرَاهُ قَالَ فِيهِنَّ: (( لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَىْءٍ قَدِيرٌ رَبِّ أَسْأَلُكَ خَيْرَ مَا فِي هَذِهِ اللَّيْلَةِ وَخَيْرَ مَا بَعْدَهَا وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا فِي هَذِهِ اللَّيْلَةِ وَشَرِّ مَا بَعْدَهَا رَبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنَ الْكَسَلِ وَسُوءِ الْكِبَرِ رَبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ عَذَابٍ فِي النَّارِ وَعَذَابٍ فِي الْقَبْرِ))‏ وَإِذَا أَصْبَحَ قَالَ ذَلِكَ أَيْضًا: ((أَصْبَحْنَا وَأَصْبَحَ الْمُلْكُ لِلَّهِ ‏))

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaahi bin Mas’uwd (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa pindi anapofika jioni akisema:

 

أَمْسَيْـنا وَأَمْسـى المـلكُ لله وَالحَمدُ لله، لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَحدَهُ لا شَريكَ لهُ،

Amsaynaa wa amsal-Mulku liLLaah wal-HamduliLLaahi. Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu

 

Tumeingia wakati wa jioni na umekuwa Ufalme ni wa Allaah, na Himdi ni Zake Allaah, hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, hali yakuwa Peke Yake, Hana mshirika (Msimuliaji akasema): Nadhani alisema pia:  

 

لهُ المُـلكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كلّ شَيءٍ قدير، رَبِّ أسْـأَلُـكَ خَـيرَ ما في هـذهِ اللَّـيْلَةِ وَخَـيرَ ما بَعْـدَهـا، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْ شَـرِّ ما في هـذهِ اللَّـيْلةِ وَشَرِّ ما بَعْـدَهـا، رَبِّ أَعـوذُبِكَ مِنَ الْكَسَـلِ وَسـوءِ الْكِـبَر، رَبِّ أَعـوذُبِكَ مِنْ عَـذابٍ في النّـارِ  وَعَـذابٍ في القَـبْر

 

Lahul-Mulku walahul-Hamdu, wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr. Rabbi as-aluka khayra maa fiy haadhihil-laylati wakhayra maa ba’dahaa, wa a’uwdhu bika minsharri maa fiy haadhihil-laylati washarri maa ba’dahaa, Rabbi a’uwdhu bika minalkasli wasuw-il kibari, Rabbi a’uwdhu bika min ‘adhaabin finnaari wa ‘adhaabin filqabri

 

Ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi, na Yeye juu ya kila kitu ni Qadiyr (Muweza). Rabb wangu, nakuomba khayr zilizomo katika usiku wa  leo, na khayr za baada yake, na ninajikinga Kwako kutokana na shari zilizomo katika usiku wa leo na shari za baada yake.  Rabb wangu, najikinga Kwako kutokana na uvivu, na ubaya wa uzee ubaya. Rabb wangu, najikinga Kwako kutokana na adhabu ya Moto na adhabu ya kaburi

 

Na alipoamka asubuhi pia alisema (kama hivyo kwa kutaja kuamka asubuhi):

 

أَصْـبَحْنا وَأَصْـبَحَ المـلكُ لله    

Aswbahnaa wa aswbahal-Mulku liLLaah  

Tumeingia wakati wa asubuhi na umekuwa Ufalme ni wa Allaah…

[Muslim (4/2088) [2723]

 

 

Share