33-Zawadi Kwa Wanandoa: Athari Za Sauti Na Harakati Katika Kuchezeana

 

Zawadi Kwa Wanandoa

 

33-Athari Za Sauti Na Harakati Katika Kuchezeana

 

الحركة والصّوت أثناء المداعبة

 

Harakati zina athari kubwa sana katika kuonyesha uzuri wa mwanamke na haswa zaidi ule wa kiroho, kwani harakati za mwanamke zinachanganya akili ya mwanamme, na mshairi Umru al-Qais anayo haya ya kusema:

 

Ikiwa kelele imeondoshwa katika nguo yake

inapelekea katika ulaini kusikokuwa na ukali

kama mchanga uliojikusanya wanatembea wazazi wawili juu yake

kwa jinsi walivyojifikiria kwa ulaini wa mshiko na wepesi wake.

 

Sauti ni chemchem ya mvuto wa hisia kali za ladha na kimapenzi, vile vile ni chanzo cha kuzungumza maneno laini ya kimapenzi, na ndani yake ni dekezo na sisimko, na sauti ya mwanamke katika kilele cha ladha ya jimai inapendeza zaidi ikiwa ni laini yenye Naghma.

 

Mwanamke kwa uzuri wa harakati zake na uchangamfu wake na uzuri wa sauti yake na utamu wake humvutia mwanamme na huteka moyo wake. Hivyo basi kuchezeana kunawafikisha katika kilele cha ladha ya tendo la Jimai.

 

Katika wanawake kuna ambao wanatoa sauti zao wakati wa Jimai na hilo halina tatizo. Asyuuti ametaja katika kitabu chake (ad-Durrul al-Manthuur) kuwa Muawiya bin Abi Sufyaan alimuita siku moja mke wake (Fakhita), akaitikia mwitiko wa kusemea puani wenye matamanio ndani yake, akaona haya na kuhisi vibaya. Muawiya akamwambia: usijali, Wallahi wabora wenu ni huu mfano wako wenye kupiga ukelele kwenye mapenzi, kunguruma na kuzungumzia puani!

 

Na katika yote haya ni msisimsho na furaha ndani yake.

 

 

 

 

Share