Skip to main content

Shaykh ‘Abdullaah Al-Ghunaymaan: Kuigawa Dini Katika Misingi Na Matawi

Kuigawa Dini Katika Misingi Na Matawi

Shaykh ‘Abdullaah Al-Ghunaymaan

Alhidaaya.com

Kuigawanya Dini kwenye misingi mikuu (uswuul) na matawi (furuu).

Misingi mikuu ya Dini (uswuul) sio ya kidhanifu au kinadharia pekee, wala hakuna utenganifu baina ya iymaan na vitendo ndani ya Uislaam.

Hakuna chochote ndani ya Qur-aan au Sunnah ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inayopendekeza kwamba misingi mikuu ni ya iymaan tu pekee na kwamba misingi midogo ni ya vitendo pekee.

Asili ya utenganifu huu umetokana na Mu’tazilah (na wafuasi wao), ambao ndio waliotenganisha namna hii: misingi mikuu na matawi.

[Shaykh ‘Abdullaah al-Ghunaymaan]