22-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Unyenyekevu Wake: Akimpandisha Kwanza Swahaba Wake Kabla Yake Katika Kipando

 

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

22-Unyenyekevu Wake Akimpandisha Kwanza Swahaba Wake Kabla Yake Katika Kipando

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

 عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ جَعْفَرٍ قَالَ: كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ إِذَا قَدِمَ مِنْ سَفَرٍ تُلُقِّيَ بِصِبْيَانِ أَهْلِ بَيْتِهِ قَالَ: وَإِنَّهُ قَدِمَ مِنْ سَفَرٍ فَسُبِقَ بِي إِلَيْهِ فَحَمَلَنِي بَيْنَ يَدَيْهِ ثُمَّ جِيءَ بِأَحَدِ ابْنَيْ فَاطِمَةَ فَأَرْدَفَهُ خَلْفَهُ قَالَ: فَأُدْخِلْنَا الْمَدِينَةَ ثَلَاثَةً عَلَى دَابَّةٍ  

 ‘Abdullaah bin Ja’far (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa pindi anaporudi safarini, watoto katika ahli yake walikuwa wakija kumpokea na kumkaribisha. Safari moja  ikawa katika hali kama hii, pindi aliporudi safarini ikawa nimemwendea mimi kwanza kabla ya mtu mwengine. Akanipandisha (katika mnyama) mimi kabla yake. Kisha akaja mmojawapo wa watoto wawili wa Faatwimah akampandisha nyuma yake ikawa hivi ndivyo sisi watatu tulivyoingia Madiynah huku tumepanda mnayma.”  [Muslim]

 

 

Share