Skip navigation.
Home kabah

Wameingiliana Baada ya Alfajiri –Nini Hukmu yake ? Na Je, Swawm Inafaa

SWALI:

 

A.W.W.NAKUTAKIENI KILA KHERI,NA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI UTUWIE WA KHERI NA BARAKA, SWALI LANGU NDIO HILI, NINA MKE NA TUPO KATIKA MWEZI MTUKUFU RAMADHANI,IMEFIKA USIKU TUMEKWENDA KULALA NA USINGIZI KUTUPITIA KTK CHUMBA HAMNA SAA,KURUPU UMEJISHTUA NA KUMTAFUTA MKE,UKU UKITAZAMA BADO KUNAONESHA GIZA,UNAJUA BADO MUDA UPO, JE SWAUMU IPO? NATAYARI IMEGUNDULIKA MUDA WADAKU UMEPITA,NA MAPENZI TAYARI KUPEYANA.KILA LA KHERI NA SWAUM NJEMA.

 







 

JIBU:

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

Waislamu wanapaswa kuzingatia sanakama kufanya jimai mke na mume kuanzia Magharibi hadi Alfajiri: amri za Mola wetu Mtukufu. Amri kama ya kufunga mwezi wa Ramadhaan ambao ni mwezi mmoja tu tulioamrishwa tubakie katika Taqwaa na kutekeleza Swawm ipasavyo. Kwa Rahma Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ameturuhusu tule, tunywe, na kuruhusiwa yote mengineyo ambayo mja amejizuia mchana wa Swawm,

((أُحِلَّ لَكُمْ لَيْلَةَ الصِّيَامِ الرَّفَثُ إِلَى نِسَآئِكُمْ هُنَّ لِبَاسٌ لَّكُمْ وَأَنتُمْ لِبَاسٌ لَّهُنَّ عَلِمَ اللّهُ أَنَّكُمْ كُنتُمْ تَخْتانُونَ أَنفُسَكُمْ فَتَابَ عَلَيْكُمْ وَعَفَا عَنكُمْ فَالآنَ بَاشِرُوهُنَّ وَابْتَغُواْ مَا كَتَبَ اللّهُ لَكُمْ وَكُلُواْ وَاشْرَبُواْ حَتَّى يَتَبَيَّنَ لَكُمُ الْخَيْطُ الأَبْيَضُ مِنَ الْخَيْطِ الأَسْوَدِ مِنَ الْفَجْرِ ثُمَّ أَتِمُّواْ الصِّيَامَ إِلَى الَّليْلِ ...))  

((Mmehalalishiwa usiku wa Swawm kuingiliana na wake zenu. Wao ni vazi kwenu, na nyinyi ni vazi kwao. Allaah Anajua kwamba mlikuwa mkizikhini nafsi zenu. Kwa hivyo Amekukubalieni toba yenu na Amekusameheni. Basi sasa changanyikeni nao na takeni Aliyokuandikieni Allaah. Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa alfajiri katika weusi wa usiku. Kisha timizeni Swawm mpaka usiku.)) [Al-Baqarah: 187] 

Sasa vipi muda wote huo usiwe wa kumtosha Muislamu kufanya yote anayoyatamani na kusubiri hadi karibu na Alfajiri ndio atake kufanya? Kwa nini usifanye hima ya kujiwekea saa ukahakikisha kuwa utaamka muda wa kutosha kamakama Alivyotuwekea sheria hiyo Muumba wetu Mtukufu. akiba pindi ukiwa umetamani kufanya jimai na mkeo? Bila ya shaka hiyo ni kujitakia mwenyewe Muislamu kujiingiza katika shida na mashaka ya kulipa kafara yake ambayo ni kuacha huru Mtumwa mmoja Muumini au kufunga miezi miwili mfululizo

Ikiwa hukujua hakika kuwa wakati wa Alfajiri umewadia unatakiwa ulipe siku hiyo na uombe maghfirah kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala). Lakini ikiwa ulijua au ulikuwa una hisia kuwa wakati umekwisha lakini tendo lile likawa limekukolea hadi ukashindwa kujizuia, basi itabidi ulipe kafara yake. Na mkeo ikiwa alitaka mwenyewe kujimai nawe pia naye itabidi atimize kafara hiyo na ikiwa ulimlazimisha basi yeye atakuwa hana kafara hiyo ila tu ailipe siku hiyo moja.  

Haipasi kufanya mchezo na amri za Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) na Mjumbe wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) khaswa katika mwezi huu mtukufu, kwani amri kama hizo ukienda nazo kinyume basi utapata matatizo duniani na akhera, na matatizo ya kidunia ni kama hayo ya kulipa kafara ambayo si rahisi na wengi hawawezi kuitekeleza.

Tunawapa nasaha ndugu zetu Waislamu wote katika mwezi huu wawe na tahadhari kubwa kufanya kinyume na ipasavyo ili kujiepusha na dhambi, kulipa kafara na kubakisha Swawm zenu katika usalama wake.

Ingia katika viungo vifuatavyo usome maelezo zaidi ya hukmu zake:

Alifanya Jimai (Kitendo Cha Ndoa) Bila Ya Kujua Kwamba Alfajiri Imeingia

Kufanya Jimai Katika Mwezi Wa Ramadhaan

Kitendo Cha Ndoa Wakati Wa Ramadhaan

Hizi ni Fataawa zote zinazohusu Kafara ya Swawm:

Kulipa Swawm Na Kafara

Na Allaah Anajua zaidi