Skip navigation.
Home kabah

Neema Ya Pepo Tuliyoahidiwa

18 Jumaadal Aakhirah 1427  14-07-2006

Tunaendelea kutaja neema za Pepo tuliyoahidiwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) ambazo zimejaa masimulizi yake katika Qur-aan na Hadiyth, 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) :

إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا ﴿31﴾ حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا ﴿32﴾ وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا ﴿33﴾ وَكَأْسًا دِهَاقًا ﴿34﴾

 لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا ﴿35﴾ جَزَاء مِّن رَّبِّكَ عَطَاء حِسَابًا ﴿36﴾

 

31. Hakika wacha Mungu wanastahiki kufuzu  

32. Mabustani na mizabibu 

33. Na wake waliolingana nao

34. Na bilauri zilizojaa

35. Hawatasikia humo upuuzi wala uongo 

36. Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha

[An-Nabaa:31-36]

Ansasema tena katika Suratul-Waaqi'ah:

  

 وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ ﴿10﴾ أُوْلَئِكَ الْمُقَرَّبُونَ ﴿11﴾ فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ ﴿12﴾ ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ ﴿13﴾ وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ ﴿14﴾ عَلَى سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ ﴿15﴾ مُتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ ﴿16﴾ يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ ﴿17﴾ بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ ﴿18﴾ لَا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ ﴿19﴾ وَفَاكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ ﴿20﴾ وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ ﴿21﴾ وَحُورٌ عِينٌ ﴿22﴾ كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ ﴿23﴾ جَزَاء بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿24﴾

  

10. Na wa mbele watakuwa mbele.  

11. Hao ndio watakaokaribishwa 

12. Katika Bustani zenye neema  

13. Fungu kubwa katika wa mwanzo

14. Na wachache katika wa mwisho. 

15. Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyotonewa.   

16. Wakiviegemea wakielekeana

17. Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele 

18. Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi

19. Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa

20. Na matunda wayapendayo

21. Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.   

22. Na Mahurul-’aini

23. Walio kama mfano wa lulu ziliohifadhiwa. 

 24. Ni malipo kwa waliyokuwa wakiyatenda

[Al-Waaqi'ah:10-24]
 

Surah hiyo tukufu inaendelea kutaja mema ya Pepo:

لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا ﴿25﴾ إِلَّا قِيلًا سَلَامًا سَلَامًا ﴿26﴾ وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ ﴿27﴾ فِي سِدْرٍ مَّخْضُودٍ ﴿28﴾ وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ ﴿29﴾ وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ ﴿30﴾ وَمَاء مَّسْكُوبٍ ﴿31﴾ وَفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ ﴿32﴾ لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ ﴿33﴾ وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ ﴿34﴾ إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاء ﴿35﴾ فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارًا ﴿36﴾ عُرُبًا أَتْرَابًا ﴿37﴾ لِّأَصْحَابِ الْيَمِينِ ﴿38﴾ ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ ﴿39﴾ وَثُلَّةٌ مِّنَ الْآخِرِينَ ﴿40﴾

  

25. Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi

26. Isipokuwa maneno ya Salama, Salama

27. Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?   

28. Katika mikunazi isiyo na miba,

29. Na migomba iliyopangiliwa, 

30. Na kivuli kilichotanda,

31. Na maji yanayomiminika  

32. Na matunda mengi 

33. Hayatindikii wala hayakatazwi, 

34. Na matandiko yaliyonyanyuliwa. 

35. Hakika Sisi Tutawaumba (Mahurul-‘aini) upya

36. Na tutawafanya vijana, 

37. Wanapendana na waume zao, hirimu moja   

38. Kwa ajili ya watu wa kuliani. 

39. Fungu kubwa katika wa mwanzo   

40. Na fungu kubwa katika wa mwisho.   

[Al-Waaqi'ah:25-40]

 

Wa kwanza kuingia Peponi ni Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):


  يقول عليه الصلاة والسلام : (( آتي الجنةَ فأستفتحُ - أي فأستأذن - فيقولُ الخازنُ : من أنتَ ؟ فأقول : أنا محمد !! فيقول : بِكَ أُمرت ألا أفتحَ لأحدٍ قبلكَ )    أخرجه الإمام مسلم في صحيحه . 

Amesema Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((Nitafika (katika mlango wa) Pepo nitaomba idhini ya kuingia, atasema milinzi: Nani wewe? Nitasema: Mimi ni Muhammad. Atasema: Kwako nimeamrishwa wala sikuamrishwa nimfungulie mtu mwingine kabla yako)) [Muslim]

 

Tutazame baadhi ya Hadiyth chache miongoni mwa nyingi  zinazosimulia neema za Pepo:

Daraja yake:
 

عن أبي سعيد الخدري عن النبي صلى الله عليه و سلم قال: ((إن في الجنة مئة درجة، ولو أن العالمين اجتمعوا في إحداهن وسعتهم)) رواه أحمد بن حنبل في مسنده

Kutoka kwa Abi Sa'iydil-Khudriy (Radhiya Allahu 'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Katika Pepo kuna daraja, na lau kama walimwengu wangelikusanyika katika mojawapo wangeenea) [Ahmad bin Hanbal katika Musnad yake]

 

عن أبي هريرة عن النبي صلى الله عليه و سلم قال: ((”إن في الجنة مئة درجة أعدها الله للمجاهدين في سبيله، بين كل درجتين كما بين السماء و الأرض، فإذا سألتم الله فاسألوه الفردوس...إلخ)) رواه البخار

Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allahu 'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Katika Pepo kuna daraja mia ambazo Ameziahidi Allah kwa wanaopigana kwa ajili yake, baina ya kila daraja mbili kama (masafa ya) baina mbingu na ardhi, kwa hivyo, mnapomuomba Allah Mumuombe (pepo ya) Al-Firdaws)) [al-Bukhaariy]

Hakuna uchafu humo:

  قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إن أول زمرة يدخلون الجنة على صورة القمر ليلة البدر ، ثم الذين يلونهم على أشد كوكب دري في السماء إضاءة ، لا يبولون ولا يتغوطون ، ولا يتفلون ولا يمتخطون ، أمشاطهم الذهب ، ورشحهم المسك ، ومجامرهم الألوة - الألنجوج ، عود الطيب - وأزواجهم الحور العين ، على خلق رجل واحد ، على صورة أبيهم آدم ، ستون ذراعا في السماء(( البخاري

Amesema Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)

((Kundi la mwanzo watakaongia Peponi watakuwa kama mwezi unapokuwa kamili. Kisha watafuatia ambao watakuwa kama nyota zinazong'ara mbinguni. Hawatakojoa, wala hawatofanya haja kubwa, wala  hawatotema mate, wala hawatopenga kamasi,  vitana vyao vya dhahabu na jasho lao litanukia kama  misk,  vyetezo vyao watatumia udi wa mawardi, wake zao watakuwa ni  hurul-'ain wenye macho makubwa. Watu watakuwa katika umbo la aina ya mtu mmoja, la  baba yao Adam (wakiwa) nchi sitini kwa urefu)) 

[Al-Bukhaariy]   

Mito yake:

عَنْ حَكِيم بْن مُعَاوِيَة عَنْ أَبِيهِ قَالَ سَمِعْت رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُول : (( فِي الْجَنَّة بَحْر اللَّبَن وَبَحْر الْمَاء وَبَحْر الْعَسَل وَبَحْر الْخَمْر ثُمَّ تَشَقَّقُ الْأَنْهَار مِنْهَا بَعْد)) وَرَوَاهُ التِّرْمِذِيّ

Imetoka kwa Hakiym bin Mu'aawiyah kutoka kwa baba yake ambaye amesema: Nimemsikia Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Katika Pepo, kuna bahari ya maziwa, na bahari ya maji, na bahari ya asali na bahari ya ulevi (wenye ladha) kisha mito itafunguka humo))

[At-Tirmidhiy]

Kwa sifa chache hizo tulizozisoma, tunatumai Insha Allah tutajitahdi kufanya mema mengi ili tulipwe neema ya Pepo ambayo humo tutaishi milele kwa furaha na amani.

Sumayyah – Mwanamke wa kwanza kufa shahidi:

Summayyah (Radhiya Allahu 'anha)   ambaye ni mwanamke wa kwanza kufa shahidi, kisa chake ni mashuhuri. Na kama tunavyojua kuwa mashahidi wangali wakiishi na kuruzukiwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) huko Peponi. Summayyah mumewe ni Yaasir (Radhiya Allahu 'anhu) na mwanawe ni 'Ammaar (Radhiya Allahu 'anhu). Walipata tabu sana ya kuteswa kwa ajili ya kuingia kwao katika Uislam. Alipoteswa Sumayyah (Radhiya Allahu 'anha) hakutetereka imani yake hata kidogo bali alivumulia mateso yote hadi akafariki akiwa ni shahidi.

Kifo chake:

Siku moja alikuwa amesimama wakati Abu Jahl anapita njia hiyo. Abu Jahl alipomwona akamrushia maneno machafu na kisha akamchoma mkuki wake katika sehemu zake za siri, akafariki kutokana na majeraha hayo.

Kusubiri kwake na mapenzi yake ya dini hii tukufu kumempa cheo cha shahidi, ambacho malipo yake ni Pepo ya kudumu milele, furaha, salama na amani.

 

 

************