Sajda Ya Kisomo - Kusujudu Wakati Wa Makruuh Inafaa Unaposoma Qur-aan?

 

Sajda Ya Kisomo - Kusujudu Wakati Wa Makruuh

Inafaa Unaposoma Qur-aan?

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Assalam alekum

 

Tunashukuru kwa kutelimisha Allaah awalipe mema awalinde na shari. Swali langu ni kuhusu kusujudu baada ya kusoma aya yenye alama ya kusujudu. Nnaposoma Qur’aani baada ya sala ya alfajiri ambako ni wakati unaochukiza kusali hadi litoke jua na nikapitia alama hiyo, je nisujudu au nisisujudu?

 

Nitashukuru kupata jibu.

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Hakika sijdah ya kisomo unaweza kusujudu wakati wowote kwani sijdah hiyo imeegemezewa kitendo fulani kinapofanywa. Hii ni kama Sijda ya kushukuru au Sunnah ya kuuamkia Msikiti (Tahiyyatul Masjid) au ya Sunnah ya wudhuu ambayo unaweza kuitekeleza wakati wowote ule hata kama ni wakati wa Makruuh.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share