Shaykh Fawzaan: Sha'baan: Hakujasihi Chochote Kuhusu Niswf Sha'baan

 

Hakujasihi Chochote Kuhusu Niswf Sha'baan

 

Shaykh Swaalih bin Fawzaan Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Hadiyth zilizopokelewa kuhusu fadhila za usiku wa Niswf Sha´baan ni Swahiyh?

 

 

JIBU:

 

Hapana. Si Swahiyh.

Hakukusihi kitu juu ya usiku wa Niswf Sha´baan wala siku ya Niswf Sha´baan.

Mtu asisimame usiku wa Niswf Sha´baan, bi maana mtu asikhusishe kusimama usiku.

Ama kuhusu yule aliyekuwa akidumu kwa kusimama tokea mwanzo asimame (kuswali) usiku wa Niswf Sha´baan kama siku zingine.

 

Ama kusema aikhusishe kwa kusimama (kuswali Swalaah ya usiku), hii ni bid´ah. Au akafunga siku ya kumi na tano ya mwezi wa Sha´baan, hii ni bid´ah. Isipokuwa yule aliyekutwa akifunga Swawm zake kama kwa mfano Swawm ya masiku meupe, afunge katika Sha´baan na siku zingine.

 

 

[Al-Mawqi’ Ar-Rasmiy li-Ma’aaliy Ash-Shaykh Ad-Duktuwr Swaalih bin Fawzaan Bin ‘Abdillaah Al-Fawzaan]

 

 

Share