036-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Twahara: Hukmu Ya Kupukusa Juu Ya Khufu Mbili

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

Mlango Wa Twahara

 

036- Hukmu Ya Kupukusa Juu Ya Khufu Mbili

 

Alhidaaya.com

 

 

Kupukusa juu ya khufu mbili kunajuzu, lakini kuosha miguu ni bora zaidi kwa mujibu wa Jamhuri ya Wanazuoni. Mahanbali wanaona kwamba kupukusa juu ya khufu mbili ni bora zaidi kwa ajili ya kuitumia ruksa. [Fat-h Al-Qadiyr (1/126), Ash-Sharh Asw-Swaghiyr (1/227), Al-Majmu’u (1/502) na Muntahaa Al-Iraadaat (1/23)].

 

La sawa ni kuwa lililo bora kwa kila mtu ni kwa mujibu wa hali yake ya uvaaji. Kwa aliyezivaa, basi apukuse juu yake na wala asizivue kwa ajili ya kumfuata Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba zake. Ama kwa asiyezivaa, basi aoshe miguu na wala asifanye uchu wa kuzivaa ili tu apukuse. [Hili ni chaguo la Shaykh wa Uislamu kama ilivyo katika Al-Ikhtiyaaraat (uk.13)].

 

Pia, asipapie kuzivua ndani ya muda wake ili tu apate kuosha miguu. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.

 

Share