011-Swahiyh Twibbin-Nabawiy: Nabiy Alitumia Aina Tatu Za Tiba Kwa Magonjwa Mbalimbali

 

Swahiyh Twibbin Nabawiy

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)

Alitumia Aina Tatu Za Tiba Kwa Magonjwa Mbalimbali

 

 

Matibabu ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mgonjwa yalikuwa ya aina tatu.

 

Ya Kwanza:  Kutumia dawa za ki atw-twabiy’iyyah (natural)

 

Ya Pili:  Kutumia dawa za ki Ilaah (Allaah)

 

Ya Tatu: Kutumia mchanganyiko kati ya aina hizo mbili.

 

Tutataja aina hizo tatu katika mwongozo wake Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Hivyo tunaanza kutaja dawa za atw-twabiy’iyyah alizoelekeza na kuzitumia (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kisha tutaje dawa za ki-Ilaah. Kisha mchanganyiko wa aina hizo za dawa.

 

Kumbuka kuwa, tunaashiria hapa kuwa ieleweke, hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  kazi iliyomleta, ametumwa kuwa ni mwongozaji, mlinganiaji, kwa Allaah na kwenye Jannah Yake,  na mtambulishaji wa Allaah na mbainishaji ummah maeneo ya kupata radhi Zake, na muamrishaji wao kufuata ardhi za Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala). Pia yeye Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni mbainishaji na mkatazaji wa mambo yanayomghadhibisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), na yeye Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  ni msimuliaji wao habari za Manabii, hali zao na  Ummah zao. Habari za kuumbwa Ulimwengu, chanzo cha kuumbwa na marejeo ya viumbe, kupotea kwa nafsi na kutengenea, na sababu zake.

 

Ama tiba ya miili: Imekuja katika kukamilisha Shariy’ah yake, na imekusudiwa lengine, kwani hutumika tu pale inapohitajika kama itawezekana kuishi bila ya tiba, kama haihitajiki hapo hima zote, na nguvu zote zitaelekezwa katika kuagua nyoyo na Roho, kulinda siha yake, na kukinga magonjwa yake, na kuzihami zisiharibike na vitu vinavyoziharibu. Na hilo ndilo kusudio la awali. Na kutengeneza mwili bila kutengeneza moyo haifai. Kuharibika mwili pamoja na kutengenea kwa moyo madhara yake ni kidogo sana. Ni madhara yanayotoweka ambapo manufaa yake ya kudumu timilifu.  Wa biLLaahi At-Tawfiyq

 

 

Share