03-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kupendeza Kuulizia Hali ya Mgonjwa Kupitia kwa Watu Wake

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب استحباب سؤال أهل المريض عن حاله

03-Mlango Wa Kupendeza Kuulizia Hali ya Mgonjwa Kupitia kwa Watu Wake

 

Alhidaaya.com

 

 

عن ابن عباسٍ رضي الله عنهما : أنَّ عليَّ بْنَ أَبي طالب رضي الله عنه ، خَرَجَ مِنْ عِنْدِ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، في وَجَعِهِ الَّذِي تُوُفِّيَ فِيهِ ، فقالَ النَّاسُ : يَا أَبَا الحَسَنِ ، كَيْفَ أصْبَحَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ؟ قَالَ : أصْبَحَ بِحَمْدِ اللهِ بَارئاً . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba 'Ali bin 'Abi Twaalib (Radhwiya Allaahu 'anhu) alitoka katika chumba cha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa anaugua kwa ugonjwa aliokufa nao. Watu walimuuliza: "Ee Abul Hasan! Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amelala (na kuamka) vipi?" Akasema: "Sifa zote anastahiki Allaah ameamka katika hali nzuri." [Al-Bukhaariy]

 

 

Share