32-Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah: Kusiwe Na Kudhuriana Wala Kulipizana Madhara

 

Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah:

 

Hadiyth Ya 32

 

لاَ ضَرَرَ وَلاَ ضِرَارَ

 

Kusiwe Na Kudhuriana Wala Kulipizana Madhara

 

Alhidaaya.com

 

Sikiliza Hadiyth:

 

 

عنْ أَبىِ سَعيدٍ سَعْدِ بْن مَالكِ بْن سِنَانٍ الْخُدريِّ رضي الله عنه  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم  قَالَ :(( لاَ ضَرَرَ وَلاَ ضِرَارَ)) حَدِيثٌ حَسَنٌ، رَوَاهُ ابْنُ مَاجَهْ وَالدَّارَقُطْنِيّ، وَغَيْرُهُمَا مُسْنَدًا. وَرَوَاهُ مَالِكٌ فِي  الْمُوَطَّإِ مُرْسَلاً عَنْ عَمْرِو بْنِ يَحْيَى عَنْ أَبِيهِ عَنْ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم  مُرْسَلًا، فَأَسْقَطَ أَبَا سَعِيدٍ، وَلَهُ طُرُقٌ يُقَوِّي بَعْضُهَا بَعْضًا. 

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd Sa’d bin Maalik bin Sinaan Alkhudriyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kusiwe na kudhuriana wala kulipizana madhara.” [Imesimuliwa na Ibn Maajah, Ad-Daaraqutwniy na wengineo na ina kiwango cha 'Musnad'. Vile vile imesimuliwa na Maalik katika Al-Muwatwaa kama 'Mursal'. Inayo mtiririko wa mapokezi kutoka kwa 'Amr bin Yahyaa, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hata ukimuacha Abuu Sa'iyd bado inayo mtiririko wa mapokezi unayoiunga mkono.]

 

 

 

 

Share