Maulidi: Kusoma Maulidi Katika Sherehe Za Ndoa Inafaa?

 

Mawlid: Kusoma Maulidi Katika Sherehe Za Ndoa Inafaa?

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Asalaam Aeikum Ndugu zangu katika Uislam

Kwanza napenda kuchukua nafasi hii, kumshukuru Allaah Subhaanahu wa Ta'aalaa kwa kunijaalia uzima na afya njema na uwezo wa kuweza kufahamu mtandao huu wa Alhidaaya. Katika siku ya leo napenda kuuliza maswali yafautayo ambayo yamekuwa yakinitatiza kichwani mwangu.

 

Je kufanya sherehe kama kusoma maulidi wakati wa ndoa ni halali? 

 

Natanguliza shukrani zangu kwa Allaah Subhaanahu wa Ta'aalaa na nyinyi pia ndugu zetu wa Alhidaaya. Wabillah Tawfiq

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho

 

Ukisoma katika mafunzo ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) utaona kuwa hakuna uzushi wa kusoma Mawlid ndani ya ndoa, na yote yanayohusiana na ndoa utayapata ndani ya vitabu hivi viwili muhimu sana katika mas-ala hayo:

 

 

Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika (Aadabu Az-Zafaaf Fiy As-Sunnat Al-Mutwahharah)

 

Zawadi Kwa Wanandoa

 

Kusoma Maulidi Kwenye Harusi Badala Kupiga Ngoma Inafaa?

 

Sherehe Za Harusi Zina Maasi Ya Mchanganyiko, Uzushi Wa Maulidi, Nyimbo Na Kujifakharisha

 

Yanayopasa Na Yasiyopasa Kutendeka Katika Ndoa

 

Yanayompasa Bwana Harusi Na Bibi Harusi Siku Ya kufunga Ndoa

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

Share