Mke Kuoa Mwanamke (Usagaji) Na Mume Kuoa Mwanamume Mwenziwe (Uliwati) Baada ya Kukubaliana

SWALI:

 

Je ikiwa mwanamke akikubali kuoa mke wa mwanaume anaempenda na mwanaume akikubali kuoa mume we na wakaelewana mahali hio inaweza kua ni ndoa tosha. Naomba jibu kwenye hayo masuali maana yake nimekosa jibu ndio mana nimependelea kuwauliza nyie mumetuzidi ilmu.

 

Ahsante sana SHUKRA

 


 

 

JIBU:

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘Alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kuoana kwa jinsi. Swali hili ndugu yetu halikukaa sawa, lau itakuwa sivyo tulivyoelewa basi utaliandika vizuri ili tupate kuelewana na kukujibu kwa njia safi kabisa.

 

Tulivyoelewa ni kuwa je, kisheria inafaa kwa mwanamme kumuoa mwanamme mwenziwe na mwanamke vivyo hivyo ikiwa wamekubaliana? Jambo hili katika sheria ni miongoni mwa dhambi kubwa hata kushinda kosa la zinaa. Kujamiiana baina ya mwanamme na mwenziwe na mwanamke na mwenziwe ni kinyume na maumbile na dhambi kubwa lenye kustahiki adhabu kali sana kisheria.

 

Kwa muhtasari, ndoa hizo hazikubaliki kisheria, ya Kiislamu.

 

Bonyeza kiungo kifuatacho upate maelezo zaidi:

 

Zinaa-Liwati

 

Na Allaah Anajua zaidi.

 

Share